Maonyesho ya Wizara ya Fedha mnazi mmoja jijini Dar es salaam - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Oct 2011

Maonyesho ya Wizara ya Fedha mnazi mmoja jijini Dar es salaam

 

Baadhi ya wananchi wa Jiji la Dar es alaam waliohudhuria maadhimisho ya Wizara ya Fedha ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara wakifuatilia jana (leo) kwa makini burudani kutoka kikundi cha Sarakasi cha Mama Afrika cha Wilayani Kinondoni kilichoshiriki katika maadhimisho hayo katika Viwanja vya Mnazi mmoja.
Maafisa wa Tanzania Investment Benk wakiwaelimisha baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es alaam waliotembelea maonyesho ya Wizara ya Fedha ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana katika Viwanja vya Mnazi mmoja juu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo katika kuleta maendeleo nchini.
Afisa Michango (Compliance Officer) wa Mfuko wa Pesheni wa PPF Jacob Sulle akitoa maelezo mbalimbali juu ya faida za fao la Elimu kwa baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es alaam waliotembelea maonyesho ya Wizara ya Fedha ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana katika Viwanja vya Mnazi mmoja .
Vijana vya kikundi cha sarakasi cha Mama Afrika cha wilayani Kinondoni wakionyesha ufundi wao katika mchezo huo jana jijini Dar es salaam wakati wa maonyesho ya Wizara ya Fedha za kuadhimisha miaka 50 Uhuru wa Tanzania Bara katika viwanja vya Mnazi mmoja.
Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dar es salaam
Afisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) akiwaelimisha baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es alaam waliotembelea maonyesho ya Wizara ya Fedha ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana katika Viwanja vya Mnazi mmoja juu taratibu za upatikanaji na ubadilishaji wa leseni za zamani ili kupata mpya.
Afisa wa Benki ya Posta wakiwaelimisha baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es alaam waliotembelea maonyesho ya Wizara ya Fedha ya Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara jana katika Viwanja vya Mnazi mmoja juu huduma mpya ya Benki ya matumizi ya simu ya mkononi kwa huduma za kibenki .
na Fullshangwe blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad