KUNDI LA MUTATI KUTOKA KENYA LAFANYA KWELI NYUMBANI LOUNGE USIKU HUU - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Sept 2011

KUNDI LA MUTATI KUTOKA KENYA LAFANYA KWELI NYUMBANI LOUNGE USIKU HUU

Kundi la Mutati kutoka Nairobi nchini Kenya likitumbuiza kwa kucheza muziki wa Salsa kwenye mgahawa wa Nyumbani Lounge unaomilikiwa na mwanamuziki Lady Jay Dee usiku huu, kundi hilo liko nchini kwa ajili ya kutoa burudani kwenye hafla ya chakula cha jioni kwa ajili ya kuchangia wanawake wenye matatizo ya ugonjwa wa Fistula katika hospitali ya CCBRT na Ukarabati wa Hospitali ya Amana zote za jijini Dar es salaam, hafla hiyo itafanyika jumamosi kwenye hoteli ya Movenpick ambapo zinatarajiwa kukusanywa zaidi ya shilingi milioni 50.
Kundi la Mutati likiendelea kupagawisha katika mgahawa wa Nyumbani Lounge usiku huu kama wanavyoonekana katika picha hii.
DJ Too Short wa Radio Clouds ni mmoja wa wadau wanaoshuhudia tukio hilo kwenye mgahawa wa Nyumbani Lounge usiku huu , kulia ni Meneja wa mgahawa wa Nyumbani Lounge Gardiner G. Habash.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad