Michezo : Mbio za Nyika zafana Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Nov 2017

Michezo : Mbio za Nyika zafana Arusha



Wachezaji wakipiga picha zawadi zao

Katibu Mkuu, Wilhelm Gidabuday akitoa Zawadi kwa Mwanariadha.

Katibu Mkuu, Gidabuday akiongea machache kabla kutoa zawadi kwa wanariadha wa mbio za Nyika katika Viwanja vya Magereza Arusha.



Yasinta Amos, Arusha.


MAANDALIZI ya kwanza ya mbio za nyika katika kusaka wanariadha watakaounda timu ya taifa yameanza kutimua vumbi katika viwanja vya magereza vilivyopo nje kidogo ya jiji la Arusha kwa timu ya JKT kufanikiwa kufanya vyema .


Kwa upande wa wanawake Mwanariadha Magdalena Shauri aliyetumia muda wa 19:54:54 huku kwa wanaume Faraja Damasi alishinda kwa muda wa 22:56:50 wote kutoka timu ya JKT .


Akizungumza katika mbio hizo katibu mkuu wa shirikisho la Riadha Tanzania ,Wilhelm Gidabudayi aliwasihi wanariadha mbalimbali wajitikeze kushiriki mbio hizo za nyika ili waweze kuonekana pindi wanapofanya vizuri ili wachaguliwe kwa hatua inayofuata ikiwemo timu ya taifa .


"Mikoa mingine nayo iwe na mashindano ya maandalizi kama haya ambayo yatasaidia na kuwajenga imara katika kupata wanariadha bora watakaochaguliwa katika timu zao za mikoa," alisema Gidabuday.


Jumla ya wanariadha 68 ,20 kati yao wanawake walichuana vikali katika mbio hizo za nyika zikiwa na lengo la Lusaka wanariadha watakaounda timu ya mkoa kwa Ajili ya mashindano ya Taifa hapo Mwakani.

Naye Msemaji wa kamati ya mbio hizo aliwalpngeza wanariadha wa timu za JKT,Polisi,Talent,Magereza kwa kuleta wachezaji wao kwa wingi pia pamoja na wachezaji binafsi ambao nao walishiriki .


"Kamati inatoa wito kwa wadhamini mbalimbali wajitokeze katika mbio tano zilizobaki ambapo mbio nyingine zitafanyika Disemba 9 katika viwanja hivyo hivyo vya Magereza," alisema Malle.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad