BUSARA ZA DIAMOND PLATNUMZ : SOMA HAPA ALICHOKIANDIKA MWANAMUZIKI NGULI WA KIZAZI KIPYA DIAMOND PLATNUMZ - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


19 Mar 2014

BUSARA ZA DIAMOND PLATNUMZ : SOMA HAPA ALICHOKIANDIKA MWANAMUZIKI NGULI WA KIZAZI KIPYA DIAMOND PLATNUMZ

Morning Africa,...SIKU YA LEO UPATAPO NAFASI,HEBU JARIBU KUFANYA MOJA YA HAYA NA UTAKUWA UMEBADILISHA MAISHA YA MTU FLANI.
-Una mlinzi?instead ya kumfokea,Hebu leo kumbuka kumsalimu na kumtakia siku njema huytu mtu anayekesha getini kulinda nyumba yako,bila shaka wengi hawafanyi hili
1:shiriki bure sehemu ya chakula chako na yeyote mwenye njaa na kuhitaji
2:Shiriki nyimbo nzuri kwa mtu mwenye huzuni ama anye feel down
3:Mfundishe mtu ,jambo analotamani kulifaham na halifaham na ni wewe pekee unafahamu
4:Una nguo ama chochote usichokihitaji tena?hapana usikitupe,mpatie yule mwenye kuhitaji
5:Una rafiki ama jamaa mpweke na pengine hana mtu wa karibu wa kushare nae yanayomsibu,make a call am text kwake,mfanye ajiskie hayupo peke yake,kwani kuna siku nawe utakuwa mpweke na utatamani mtu wa kuzungumza nae
6:Panga ku donate damu,damu yako kidogo inaweza ikaokoa maisha ya mtu sehemu flani..
7:Saidia mzee,ama mtoto kuvuka barabara.
8:Ambia rafiki,family member ama mtumishi ni kiasi gani una mwappreciate
9:Saidia mji wako kuwa msafi,si kazi kubwa kuokota kipande cha uchafu na kuweka sehemu husika
10:Mpigie mzazi wako na kumwambia ni kiasi gani unampenda
11:Motivate mtu flani atimize ndoto zake
12:Jipe amani ya moyo kwa kusamehe
13: la mwisho,jifanyie wewe mwenyewe,Acha kufanya kitu kibaya ulichokuwa unaufanyia mwili wako,pengine uvutaji wa sigara,ulevi wa kupita kiasi etc
....HAIJALISHI NI KIDOGO KIASI GANI UTAKACHOKIFANYA,KUWEKA TABASAMU KWA MTU,NDICHO KINACHO MATTER ...Siku njema 

kutoka(fB page yake)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad