Na. Saidina Msangi, WF, Chalinze
Timu ya Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha, imefika Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani kwa ajili ya kutoa elimu ya fedha kwa wananchi itakayo wawezesha kuepukana na mikopo umiza pamoja na kujifunza kuhusu riba, mikopo, dhamana na uwekezaji.


Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya Fedha Bw. Stanley Kibakaya, akitoa elimu ya fedha kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kutumia taasisi za fedha zilizosajiliwa wanapochukua mikopo ili kuwawezesha kuondokana na mikopo umiza pamoja na umuhimu wa kuzingatia mapato na matumizi ili wajiwekee akiba, wakati Maafisa wa Wizara ya Fedha walipokuwa wakitoa elimu ya fedha kwa wananchi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Chalinze.



Baadhi ya wananchi wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa na Maafisa kutoka Wizara ya Fedha waliowasili kutoa elimu ya fedha kwa wananchi, kuhusiana na usimamizi wa fedha binafsi, dhamana za mikopo, riba pamoja na uwekezaji, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Chalinze.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Chalinze -Pwani)
No comments:
Post a Comment