Matukio :Tamasha la Pasaka kutikisa kanda ya ziwa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Mar 2018

Matukio :Tamasha la Pasaka kutikisa kanda ya ziwa



Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion inayoandaa Tamasha la Pasaka akizungumza katika moja ya mikutano yake na waandishi wa habari kuelezea maandalizi ya Tamasha hilo litakalofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Aprili 1 na Kwenye uwanja wa Halmashauri mjini Bariadi mkoani Simiyu.
Mwimbaji Jesca Honore akithibitisha kushiriki katika tamasha hilo kushoto ni Chrstopher Mwahangila mwimbaji mwingine ambaye atashiriki katika tamasha hilo mkoani Mwanza na Simiyu na katikati ni Jimmy Charles mmoja wa waratibu wa tamasha hilo.
Mwimbaji Upendo Nkone akithibitisha kushiriki katika tamasha hilo kushoto ni Mwimbaji Joshua Mlelwa ambaye pia atakuwepo katika tamasha hilo katikati ni Ufo Saro mmoja wa waratibu wa Tamasha hilo.
Mwimbaji Martha Baraka akitibitisha kushiriki katika tamasha hilo kutoka kushoto ni Jimmy Charles mmoja wa waratibu wa Tamasha hilo na katikati ni Mzee Rainfred Masako mmoja wa Viongozi wa Dira TV.
Mwimbaji Paul Clement akizungumza kuhusu maandalizi yake na kuthibitisha kwamba yuko tayari kwa ajili ya kutumbuiza katika Tamasha a Pasaka Kanda ya Ziwa kushoto ni Mwimbaji mwenzake Beatrice Mwaipaja .
Mwimbaji Christopher Mwahangila akifanya vitu vyake katika moja ya video zake alizowahi kurekodi.

.................................................................................................

Ni siku nne zimebaki kengele ya Tamasha la Pasaka zinahesabika. Ni Aprili Mosi, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Mara nyingi Tamasha la Pasaka limekuwa likifanyika jijini Dar es Salaam safari hii Msama Promotion imeamua kulifanya tamasha hilo Kanda ya Ziwa. Hivyo Pasaka hii, wapenda muziki wa injili wa Kanda ya Ziwa na viunga vyake watapata burudani ya nyimbo za kumsifu na kumtukuza Mungu huku wakipata mahubiri kwa njia ya uinjilisti wa nyimbo.

Aprili Mosi ni CCM Kirumba, Aprili Pili Tamasha la Pasaka litachukua nafasi Uwanja wa Halmashauri, mkoani Simiyu ambako nako watasheherekea kwa nyimbo za injili.

Wakati siku zikikaribia kuelekea Tamasha la Pasaka kwa mkazi wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa jumla ni kuendelea kumuomba Mungu ili aendelee kukupa uzima na afya njema.Waandaaji wa tamasha hilo, Kampuni ya Msama Promotion, mwaka huu wameamua kuweka vionjo tofauti ili kuhakikisha tamasha hilo linafanyika na kuacha historia kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa.

Kila mwanamuziki aliye kwenye chati, nyimbo zake za kumsifu na kumtukuza Mungu zikiwa zinatamba na kusikika, atakuwemo kuburudisha mashabiki wake na kubwa zaidi ni kwamba kuna baadhi ya waimbaji wataimba wakipiga vyombo vya muziki Live ili kuleta ladha na burudani zaidi katika tamasha hilo..

Kwa mujibu wa waandaji wa Tamasha la Pasaka, mwimbaji Rose Muhando atazindua albam yake mpya “Usivunjike Moyo” kati ya waimbaji wengi kutoka hapa nchini Tanzania na nje watakaofanya mambo makubwa katika tamasha hilo.

Inafahamika kuwa Rose Muhando huwa hahitaji utambulisho. Ni mwanamuziki mkubwa kati ya waimbaji wa muziki wa injili ambaye Muumba wa Mbingu na Ardhi amenyanyua kipaji cha kuimba kilichoambatana na sauti maridadi. Muziki wa Rose Mhando unapopigwa wapo ambao wanasimamisha shughuli zao kwa muda ili kumsikiliza kwanza.

Kwa Rose Mhando mwenyewe anajua ukubwa wa Tamasha la Pasaka. Wakati anazungumzia tamasha hilo ameeleza wazi amejiandaa vya kutosha. Hivyo atakuwa Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kuonesha kile ambacho amewaandalia. ambapo pia atazindua albamu yake mpya inayoitwa

Imekuwa kawaida kwa matamasha ya Pasaka kuleta wanamuziki kutoka nje ya nchi. Kwa taarifa tu ni kwamba atakuwepo Ephrem Sekereti kutoka Zambia. Mashabiki wa muziki wa Injili wanamfahamu vema Sekeleti na ubora wa kazi zake.

Wakazi wa Mwanza na Simiyu ni zamu yenu mwaka huu kupitia Tamasha la Pasaka kuweka historia ya kumshuhudia mwanamuziki Sekereti akitoa burudani tena ndani ya ardhi ya Tanzania. Karibu Sekereti wakazi wa Mwanza na Kanda ya Ziwa wanakusubir.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad