Elimu : Waziri Jafo - Wataalamu wa Maji zaidi ya 4,000 wanahitajika TAMISEMI - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


13 Jan 2018

Elimu : Waziri Jafo - Wataalamu wa Maji zaidi ya 4,000 wanahitajika TAMISEMI



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati) akiwasili kwenye Chuo cha Maji tayari kwa kutunuku Shahada na Stashahada katika mahafali ya Tisa ya Chuo hicho.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati) akishiriki kwenye maandamano ya Kitaaluma kuelekea uwanja wa Sherehe Mahafali ya Tisa ya Chuo cha Maji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo akizungumza na wahitimu wa Chuo cha Maji, Wakufunzi na wageni waalikwa(hawapo pichani) wakati wa Mahafali ya Tisa ya Chuo hicho.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo akitoa Cheti kwa mwanafunzi wa kike aliyefanya vizuri Kitaaluma katika ngazi ya Astashahada.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati) katika Picha ya Pamoja na Uongozi wa Chuo cha maji.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani Jafo(Katikati aliyekaa) katika Picha ya Pamoja na wanafunzi waliohitimu Shaada ya Uhandisi na Rasilimali za Maji na Umwagiliaji katika Chuo cha Maji.






Nteghenjwa Hosseah, Dar es Salaam.




Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amesema mahitaji ya wataalam wa Maji kwa sasa katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Nchini ni kati ya elf nne – hadi elfu saba.


Jafo ameyasema hayo wakati alipokuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya Tisa ya Chuo cha Mji yaliyofanyika Tar 11/01/2018 katika chuo hicho kilichopo Jijini Dar es salaam.


“Taalum hii ni muhimu sana katika ustawi na Afya ya wananchi wetu kote Nchini, uhakika wa kupata maji salama bado ni changamoto kubwa kutokana kutokuwa na miundombinu ya Uhakika na zaidi ni wataalamu wachache waliopo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa” Alisema Jafo.


Aliongeza kuwa Nipongeze chuo hiki cha maji kwa kutoa Shahada kwa mara ya kwanza katika Historia ya Chuo hiki, hapo awali hapakuwa na Ngazi ya Shahada hivyo wataalamu wengi waliishia ngazi ya Stashahada ambapo mara nyingine ilihitajika Utaalamu zaidi kutokana na changamoto za kiutendaji katika maeneo mbali.


“Kwa sasa mmejibu changamoto hii katika Sekta ya Maji kwa kufanikisha kutoa wahitimu wa Ngazi ya Shahada haya ni mafanikio kwa Chuo, kwa Wahitimu na Taifa kwa Ujumla nawapongeza sana na nawakaribishe katika Kulitumikia Taifa hili kwa sababu ujuzi mlioupata unahitajika sana” Alisema Jafo.


Akizungumza na Wahitimu, Wakufunzi na wageni waalikwa Waziri Jafo alisema Kuhitimu ni jambo moja lakini jinsi gani mnaenda kutumia Taaluma yenu ni jambo lingine, mnatakiwa mkafanye kazi kwa weledi wa hali ya Juu huku, muwe waadilifu na mtumie vuzuri rasmilimali za Umma.


“Nyie sasa mtakwenda kuwa wajumbe kwenda bodi za Zabuni katika maeneo mtakayofanyia kazi mkapambane na rushwa katika miradi ya maji, ili miradi iweze kutekelezwa kwa kiwango na thamani ya Fedha ikaonekane misende kuwa sehemu ya ubadhirifu wa mali za Umma, Rushwa hupofusha maji na huondoa weledi wako mkajihadhari sana na Rushwa alimalizia Waziri Jafo.


Akizungumza katika Mahafali hayo Mkuu wa Chuo cha Maji Shija Kazumba alisema jumla ya wanafunzi 248 wamefuzu Stashahada-Uhandisi wa usambazaji wa maji na usafi wa mazingira wakati wahitimu 127 wamehitimu hyrolojia na Uchimbaji wa visima, wahitimu 23 wamehitimu haidrolojia na Mateorolojia, wahitimu 12 wamehitimu Stashahda ya Teknolijia ya Maabara na ubora wa maji na wahitumu 50 ni wa Stashahada, Uhandisi Umwagiliaji


Katika Ngazi ya Shahada waliofuzu na kustahili kupata shahada ya Uhandishi WA Rasilimali maji na Umwagiliaji ya Chuo cha Maji kwa mara ya kwanza ni wanafunzi 54.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad