Matukio : Kutoka Bungeni Dodoma Leo, 09:11:2017 - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


9 Nov 2017

Matukio : Kutoka Bungeni Dodoma Leo, 09:11:2017






Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akimsikiliza Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mhe.Freeman Mbowe wakati wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu leo Bungeni Mjini Dodoma.

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akijibu maswali mbalimbali ya wabunge wakati wa maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiteta jambo na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Mbunge wa Viti Maalum(CHADEMA) Mhe.Dk Imaculate Semesi wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Mbunge wa Bukombe(CCM) Mhe.Doto Biteko akiuliza swali wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba akijibu maswali mbalimbali ya wabunge wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.William Ole Nasha akitolea ufafanuzi hoja mbalimbali za wabunge wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Wanafunzi wa kidato cha sita wa Shule ya sekondari Dodoma wakiwa bungeni kujifunza shughuli mbalimbali za bunge ilo wakati wa kikao cha tatu cha mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai akiongoza mkutano wa tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Mjini Dodoma.

Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof Joyce Ndalichako akiwasilisha kauli ya Serikali kuhusu udahili na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka 2017/2018 Bungeni mjini Dodoma.


Picha zote na Daudi Manongi.MAELEZO,DODOMA.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad