Matukio : TGGA Yatoa somo Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Kisarawe - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Jun 2017

Matukio : TGGA Yatoa somo Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Kisarawe






Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtera Mwampamba (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Kamishna wa Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA) Makao Makuu, Rose Majuva kuhusu kazi zinazofanywa na chama hicho ikiwemo kuwapa uwezo wanawake wa kujitambua na kujiamini alipokwenda kuzindua Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wilayani humo.

Majuva aliwaasa wanawaje kuacha kutumia mikopo ya benki kuchezea ngoma bali waitumie kujiendeleza kibiashara na kuwa na tabia ya kulipa kwa wakati mikopo hiyo. Pia aliwaeleza mbinu mbalimbali za kufanya biashara na miiko yake. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDAKAMANDA WA MATUKIO BLOG
Wananchi wakisikiiza kwa makini maelezo kutoka kwa Mkufunzi wa TGGA, Valentina Gonza jijsi ya kutengeneza jiko la kutumia mwanga wa jua kupikia vyakula mbalimbali kwa gharama nafuu wakati wa maonesho yaliyofanyika wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo mjini Kisarawe.

Girl Guides wa TGGA, wakitengeneza Green House ya kupanda matunda na mbogamboga majumbani waliposhiriki uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wilayani Kisarawe. Kutoka kushoto ni Rachel Baganyire kutoka Uganda, Michelle kutoka Rwanda na Happy Mshana wa Makao Makuu ya TGGA, Dar es Salaam.
Kamishna wa Makao Makuu ya TGGA, Rose Majuva (kulia) akisoma maadili ya kiongozi anavyotakiwa awe wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Wilaya ya Kisarawe.
Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Ruth Namatanga akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam,Rehema Kijazi akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Valentina Gonza akigawa karatasi ya kupigia kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
Mkufunzi wa TGGA, Makao Makuu Dar es Salaam, Ruth Namatanga akikusanya kura kwa Wajasiriamali wakati wa uchaguzi wa viongozi wa Jukwaa hilo.
Baadhi ya viongozi wa TGGA wakihesabu kura wakati wa uchaguzi huo
Viongozi wa TGGA wakiwa kwenye banda lao wakati wa maonesho yaliyofanyika wakati wa uzinduzi wa Jukwaa hilo mjini Kisarawe
Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtera Mwampamba (kulia), akiangalia kiroba cha mkaa uliotengenezwa kiasili kwa kutumia taka mbalimbali alipokuwa akitembelea mabanda ya wajasiriamali kabla ya kuzindua Jukwaa hilo. Kushoto ni Gifti Mbaraka wa banda hilo la Vijana Wasiriamali Wakulima Kisarawe. Katikati ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kisarawe, Mussa Gama.
Mwampamba akiangalia bidhaa mbalimbali za wajasiriamali
Girl Guides kutoka Madagascar akijitambulisha wakati wa mkutano wa Jukwaa hilo. Kutoka kulia ni Rachel Baganyire kutoka Uganda na Michelle kutoka Rwanda. Vijana hao wapo nchini kwa miezi sita katika programu ya kubadilishana uozefu katika masuala ya utamaduni, uongozi na ujasiriamali
Mkufunzi kutoka Makao Makuu ta TGGA, Happy Mshana akielezea jinsi alivyopata uzoefu alipoiwakilisha TGGA kwenye mafunzo ya kubadilisha uzoefu nchini Madagascar

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad