Maisha : Waziri, Mhe. Jenista Mhagama Aipongeza Mfuko wa Jamii wa LAPF - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


13 Mar 2017

Maisha : Waziri, Mhe. Jenista Mhagama Aipongeza Mfuko wa Jamii wa LAPF



Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu) Bi.Jennista Mhagama akizungumza katika mkutano mkuu wa9 wa wadau wa mfuko wa hifadhi ya watumishi wa serikali za mita,LAPF jijini Arusha

Mkurugenzi wa KeyMedia Agency ya jijini Arusha akiwa katikati Bi.Barbra Keiya wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa LAPF, kampuni hiyo ilibeba jukumu la kualika vyombo vya habari kwaajili ya mkutano huo

Wakurugenzi wa KeyMedia Agency ya jijini Arusha Bi.Anna na Barbra wakiwa katika picha ya pamoja na mameneja wa LAPF

Baadhi ya wafanyakazi wa KeyMedia Agency ya jijini Arusha wakiwa katika picha ya pamoja

Na Pamela Mollel,Arusha


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu) Bi.Jennista Mhagama amewataka vijana kujiepusha na madawa ya kulevya ili utekelezaji wa dhana ya Tanzania ya viwanda ilete ajira kwa vijana wenye nguvu


Aliyasema hayo jijini Arusha wakati akifunga mkutano mkuu wa9 wa wadau wa mfuko wa hifadhi ya watumishi wa serikali za mita,
LAPF uliohudhuriwa na wadau wa mfuko huo


Alisema kuwa kwa sasa serikali imedhamiria kuwainua idadi kubwa ya vijana waliona ujuzu mdogo kwa kuwajenge uwezo kupitia mafunzo mbalimbali katika vyuo vilivyopo nchini


''Udhibiti mkubwa wa madawa ya kulevya unahitajika kwa vijana wetu ili kutengeneza taifa lenye nguvu ya kufanya kazi ''alisema


Aliongeza kuwa asilimia kubwa ya watanzania hawana ujuzi wa kutosha hivyo basi serikali ya awamu ya 5 imejipanga ipasavyo kuhakikisha vijana wanapata ajira kupitia viwanda


Hata hivyo aliipongeza mfuko wa LAPF kwa kazi nzuri wanayofanya huku akiitaka mifuko yote ya kijamii hapa nchini ihakikishe kuwa ifikapo 2025 inakuwa na wanachama wengi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad