Maisha :Watetezi wa Haki za Wanawake wapewa mafunzo Jinsi ya kufanya utetezi katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


5 Jan 2017

Maisha :Watetezi wa Haki za Wanawake wapewa mafunzo Jinsi ya kufanya utetezi katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa

Nasieku Kisambu Mkurugenzi wa Mipango Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) akizungumza katika mafunzo ya Haki za Wanawake na Jinsi ya kufanya utetezi katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa yakiwa na lengo la kuongeza uelewa wa misingi ya kulinda na kutetea haki za wanawake na watoto Kitaifa , Kikanda na Kimataifa.


Kuelewa mifano iliyopo katika Kanda, Kikanda na kimataifa inayolinda haki za wanawake , Haya ni mafunzo yanayolenga kujenga uwezo wa Taasisi zinazotetea haki za wanawake kutumia fursa zilizopo katika mikataba, Taasisi na mifumo ili kuweza kubadilisha sera na sheria kandamizi na kutetea haki za wanawake.


Mafunzo hayo yanayofanyika kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam yameandaliwa na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) na kwa ushirikiano na mashirika mengine yanayotetea haki za wanawake na watoto ambapo wadau mbalimbali kutoka katika taasisi hizo wameshiriki katika mafunzo hayo

Maria Matui Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania (TAWLA) akifungua mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam.

Mkufunzi wa Mafunzo hayo Dk. Clemence Mashamba akitoa mada wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea kwenye hoteli ya Courtyard Upanga jijini Dar es salaam.

Christina Kamili Mkurugenzi Mtedaji wa Shirika la Tanzania Network Of Legal And Providers akifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Mkufunzo wa Mafunzo hayo Dk. Clemence Mashamba hayupo pichani.

Baadhi ya washiriki mbalimbali wa mafunzo hayo wakifuatilia mada zilizokuwa kititolewa na mkufunzi huyo.

Christina Kamili Mkurugenzi Mtedaji wa Shirika la Tanzania Network Of Legal And Providers akifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Mkufunzo wa Mafunzo hayo Dk. Clemence Mashamba hayupo pichani.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada mbalimbali katika mafunzo hayo.

Mkufunzi wa mafunzo hayo Dk Clemence Mashamba akiwa na Dotto Joseph Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya National Oganization For Legal Assistance (Nola)

Maria Matui Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake Wanasheria Tanzania TAWLA akipitia nyaraka za mmbalimbali za mafunzo hayo.

Washiriki wa Mafunzo hayo wakiwa katika picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad