Meneja
wa Mradi wa Umeme wa Makambako – Songea, Didas Lyamuya (katikati),
akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard
Kalemani (kulia) na Mbunge wa Makambako, Deo Sanga (kushoto), kuhusu
maendeleo ya Mradi huo wakati wa ziara ya Naibu Waziri mkoani Njombe
hivi karibuni
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani, akizungumza na wananchi
wa Kijiji cha Lyamkena kilichopo Makambako mkoani Njombe hivi karibuni,
wakati akiwa katika ziara kukagua miradi ya umeme.
Wananchi
wa Kijiji cha Lyamkena, Wilaya ya Makambako mkoani Njombe,
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani
(hayupo pichani), wakati wa ziara yake mkoani humo hivi karibuni,
kukagua miradi ya umeme.
Wananchi
wa Kijiji cha Lyamkena, Wilaya ya Makambako mkoani Njombe,
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani
(hayupo pichani), wakati wa ziara yake mkoani humo hivi karibuni,
kukagua miradi ya umeme.
Na Veronica Simba - Makambako
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani ametoa ahadi kwa wakazi
wa Kijiji cha Lyamkena kilichopo Makambako mkoani Njombe, kuwa
watasherehekea sikukuu ya Krismas hapo Desemba 25 mwaka huu wakiwa na
umeme.
Dk
Kalemani aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi husika jana
kijijini hapo, mbele ya Mbunge wa Makambako Deo Sanga, akiwa katika
ziara kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme.Naibu Waziri
alimwagiza Meneja anayesimamia Mradi wa Umeme wa Makambako – Songea,
Didas Lyamuya, kuhakikisha kazi ya kutandaza nyaya inafanyika usiku na
mchana ili umeme uwake katika eneo hilo kufikia Desemba 25.
“Tumekubaliana
na Meneja, amejipanga kuanzia wiki ijayo wataanza kutandaza nyaya na
watakamilisha ndani ya siku 10,” alifafanua.Aidha, Dk Kalemani
alimwagiza Meneja huyo kuviingiza katika Mradi huo mkubwa wa umeme,
vijiji vya Kihumba na Katani ambavyo vilisahaulika, ili vipatiwe umeme
sambamba na maeneo mengine yote kama yalivyoainishwa katika Mradi.
Awali,
akitoa taarifa ya maendeleo ya Mradi husika kwa Naibu Waziri, Lyamuya
aliahidi kukamilisha kazi yote na kukabidhi rasmi Mradi ifikapo mwezi
Juni mwakani ambayo ni miezi mitatu kabla ya muda uliopangwa yaani
Septemba 2018.Kufuatia ahadi hiyo, Naibu Waziri alimpongeza kwa kufanya
kazi kwa bidii na kumtaka aendelee na ari hiyo ili wananchi wa Mikoa ya
Njombe na Ruvuma wapate umeme utakaowasaidia kuendesha shughuli
mbalimbali za kimaendeleo na kuinua uchumi wao.
Kwa
upande wake, Mbunge wa Makambako, Deo Sanga, alimshukuru Naibu Waziri
Kalemani kwa niaba ya Serikali kwa jitihada ambazo Wizara yake imekuwa
ikizifanya ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu ya umeme.
Aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ili azma ya wananchi
wake kupatiwa umeme itimizwe kama ilivyopangwa.