Utalii : TANAPA na Wadau wa usafiri wa Anga kukuza sekta ya Utalii Nchini - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


22 Nov 2016

Utalii : TANAPA na Wadau wa usafiri wa Anga kukuza sekta ya Utalii Nchini



Ndege ya shirika la Precision Air ikiwa tayari imetua katika uwanja wa Seronera ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoa wa Mara ikiwa na watalii 43 kutoka nchi Afrika Kusini iliyowachukua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere hatua inayoelezwa kuokoa muda na kupunguza gharama.


Abiria wakishuka kutoka kwenye ndege ya shirika la Precision Air ambayo imeanza safari za moja kwa moja kutoka jijini Dar es Salaam na Zanzibar hadi kwenye hifadhi hiyo.


Watalii wakifurahi baada ya kutua salama kwenye uwanja wa Seronera ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.


Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa nchini(katikati)akiwa katika picha ya pamoja wa wafanyakazi wa shirika la Precision Air,kulia kwake ni Kapteni Benjamini Maluli na kushoto kwake ni Murtazir Ghulamhusein




Watalii wakipata picha ya pamoja ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti


Meneja Uhusiano wa Tanapa,Pascal Shelutete akifafanua umuhimu wa ndege kubwa za abiria kwenda moja kwa moja kwenye hifadhi za taifa kutakavyoinua sekta ya utalii nchini.


Ndege ya shirika la Precision Air ikiruka kutoka uwanja mdogo wa Seronera  ndani ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoa wa Mara.


Makundi makubwa ya wanyama aina ya Nyumbu ni miongoni mwa vivutio ndani hifadhi ya Serengeti


Tembo wenye miili mikubwa wakiwa ndani ya Hifadhi ya Serengeti


Fisi wakijipooza joto kwenye dimbwi la maji.






Wafanyakazi wa Sence of Afrika wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa tayari kuwapokea wageni wanaotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.



Na Dixon Busagaga.
 
SHRIKA la Hifadhi za Taifa  (TANAPA) limeanza jitihada kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na  Mashirika makubwa ya ndege ,kuona ni namna gani yanaweza kusaidia katika kuinua sekta ya utalii hapa nchini.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi na Hifadhi za taifa ,ndege aina ya ATR namba 5H-PWE inatua katika uwanja wa ndege uliopo katika Hifadhi ya taifa ya Serengeti huku ikiwa na abiria 45 kutoka nchini Afrika kusini waliofika kwa ajili ya Utalii.

Ndege hii mali ya kampuni ya Shirika la ndege la Precision Air imetua majira ya saa 11:40 juzi jioni ikiwa ni ishara ya uzinuzi rasmi wa safari za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi katika hifadhi ya Serengeti ambazo sasa zitafanyika mara tatu kwa juma.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete anasema kuanza kwa safari za ndege katika hifadhi hii kutaongeza idadi ya watalii ambao kwa sasa watatumia muda mfupi kufika hifadhini.

Kwa upande wa kampuni zinazojishughulisha na biashara ya utalii nchini hatua ya shirika la ndege la Precision Air kufanya safari za moja kwa moja hadi hifadhi ya Serengeti ina maana gani kwao.

Hatua hii ikalisukuma Shirika la Hifadhi za Taifa Tanapa ,sasa kuangalaia uwezekano wa kuendelea kutoa ushawishi kwa mashirika mengine ya ndege kufanya safari zao katika hifadhi zilizopo kusini mwa Tanzania.

Kuhusu usalama katika viwanja vya ndege vilivyoko katika Hifadhi za taifa Shelutete ameyaondoa hofu mashirika ya ndege na kwamba viwanja vimekaguliwa na vina uwezo wa kupokea ndege mbalimbali.

Kuanza kwa safari za ndege za moja kwa moja hadi katika hifadhi za taifa ni fursa nyingine kwa Tanapa na kampuni za Utalii nchini kwa kuongeza idadi ya wageni watakaotembelea vivuito vya utalii na kuongeza pato la taifa kupitia fedha za kigeni.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad