Matukio : RC Iringa ampongeza salim abri Asas kusaidia kuokoa maisha ya majeruhi wa ajali - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


6 Nov 2016

Matukio : RC Iringa ampongeza salim abri Asas kusaidia kuokoa maisha ya majeruhi wa ajali


Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa Salim Abri Asas (kushoto) akimkabidhi mgeni rasmi katika maadhimisho ya wiki ya nenda kwausalama kwa mkoa wa Iringa leo , mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza zawadi maalum ya kamati ya usalama barabarani mkoa kutokana na mchango wake mkubwa kwa kamati hiyo

Kitengo cha usalama barabarani mkoa wa Iringa wakijiandaa kutoa elimu katika viwanja vya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani
Baadhi ya wananchi na watu wenye ulemavu wakiwa katika viwanja vya maadhimisho hayo



Mwakilishi wa wakala wa barabara mkoa wa Iringa akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Iringa na watu mbali mbali waliotembelea banda hilo kuona shughuli zinazofanywa



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza akitoa hotuba yake leo wakati wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani ,kulia kwake ni mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa Salim Abri Asas na katibu wake RTO Leopold Fungu wakifuatilia hotuba hiyo



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza akihamasisha upimaji afya na uchangiaji damu katika banda la HOspitali ya Rufaa mkoa wa Iringa ambao walishiriki maadhimisho hayo ya wiki ya nenda kwa usalama mkoa wa Iringa leo kwenye viwanja vya stendi kuu ya mkoa



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wadau na kamati ya usalama barabarani mkoa wa Iringa mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo katika viwanja vya Stendi kuu , kushoto kwake ni katibu tawala wa mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu ,Kaimu RPC , DC Iringa Richard Kasesela ,Naibu meya wa Manispaa ya Iringa Mh. Lyata na kutoka kushoto wa kwanza ni katibu wa kamati ya usalama barabarani mkoa Leopold Fungu na mwenyekiti wake wa kamati Salim Abri Asas



Dc Iringa Richard Kasesela akipata maelezo katika banda la zima moto



Afisa habari mkoa wa Iringa Denis Gondwe akipokea maelekezo toka kikosi cha usalama barabarani .
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza akiwa akishirikiana na mwanafunzi wenye ulemavu wa ngozi toka Lugalo sekondari Semeny Sadick kuzima moto uliowashwa na kikosi cha zimamoto na uokoaji ili kutoa elimu kwa wananchi juu ya uzimaji moto baada ya kikosi hicho kutoa elimu katika shule zote za Manispaa ya Iringa



Mwanafunzi Semeny akizima moto



Wasanii toka Mkwawa Magic Site Iringa wakionyesha ujuzi wa kucheza na nyoka aina ya chatu



Askari wa usalama barabarani mkoa wa Iringa maarufu kwa jina la bibi akimpa pesa msanii wa Mkwawa Magic Site



Msanii toka kikundi cha Mkwawa Magic Site akicheza mbele ya mgeni rasmi

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad