Matukio : Mkuu wa Wilaya Handeni, Mhe. Godwin Gondwe apiga marufuku ufugaji Holela - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


22 Oct 2016

Matukio : Mkuu wa Wilaya Handeni, Mhe. Godwin Gondwe apiga marufuku ufugaji Holela

Mkuu wa Wilaya Mh. Godwin Gondwe akizungumza na wananchi wa kijiji cha  Chogo  wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akifutiwa na Mh.Aabdalla Pendeza Diwani wa Kata ya Kabuku Ndani na wakwanza kushoto ni mwenyekiti wa kijiji cha chogo. 
 Mkuu wa Wilaya ,Mkurugenzi Mtendaji na viongozi wengine kutoka Halmashauri wakitazama moja ya eneo laKitalu cha kuoteshea miti ya malimao mkulima baada ya kupitia shamba na kuona uharibifu uliofanyika.
baadhi ya wananchi kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku ndani.  
 mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya handeni akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chogo kata ya Kabuku Ndani.
  Mmoja kati ya wafugaji waliopo katika kijiji cha Chogo Bw. Masanja akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi na  wananchi wote kwa ujumla.

 ======  =======  ========
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe  na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe wamepiga marufuku ufugaji holela. Tamko hilo limetolewa baada ya uongozi wa kijiji cha Chogo Kata ya Kabuku Ndani kuomba Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji kuwasaidia kuondoa wafugaji waliovamia katika kijiji chao na kuharibu mazao ya kilimo ya wananchi wa kijiji hicho.

Akizungumza na wananchi hao Mkuu wa wilaya aliwaeleza wananchi kuwa kila sehemu kuna taratibu na sheria zake namna ya kuishi. “ni marufuku kuchunga mifugo kwenye maeneo ya hifadhi ya misitu ya Serikali au ya Kijiji kwa maana  ni kosa akipatikana mtu wa namna hiyo kamateni peleka polisi na mimi nifahamu”alisema, na pia ni marufuku kuchukua mifugo kwenda kuchunga kwenye shamba  la mwenzako kuwepo na  mazao au  hakuna ni kosa kamateni mtu wa namna hiyo  peleka polisi, hata kama mwenye shamba amekwisha vuna isipokuwa kwa idhini ya mwenye shamba pekeyake.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni aliwaeleza wananchi  kwamba ulinzi wa mali za Chogo  ni wanachogo wenyewe, na mgogoro wa wakulima na wafugaji ni wetu sote, Aliwaeleza kwamba walishindwa kuchukua tahadhari mapema pindi wafugaji hao walipoingia miezi mine iliyopita kwa sababu eneo lao lina mpango bora wa matumizi ya ardhi. 

Aidha aliwaeleza wananchi kuwa, amewataka  Watendaji wa Kata na Vijiji kuleta orodha ya mifugo iliyopo kwenye maeneo yao na waeleze uwezo wa ardhi iliyopo kuweza kuhimili idadi ya mifugo iliyopo kwa mujibu wa mpango wa ardhi uliowekwa katika maeneo yao ili kugungua  kama kunamifugo imezidi au haijazidi, “Tarehe 29/10/2016 nitapata orodha ya Halmashauri nzima kwa kata 21 na  Vijiji 91” alisema. 

Mfugaji wa mwanzo ambae atakuwepo katika kijiji husika kwa kumkaribisha ama la kama idadi ya mifugo aliyokuwa nayo inakidhi viwango atabaki, lakini kwa mfugaji atakaye zidisha kiwango cha mifugo basi ataondolewa ili aende  kutafuta mahali kwingine na marufuku kukaribisha mfugaji mwingine alisema Mkurugenzi.

Mwenyekiti wa kijiji cha Chogo aliwaeleza viongozi kuwa wafugaji hao waliingia kwenye maeneo yao bila kufuata utaratibu, wameleta uharibifu wa mazao napindi wanapohitajika kwenye vikao ili wapewe utaratibu wanakaidi kufika. Alieleza kuwa eneo ambalo limetengwa kaajili ya mifugo lipo eneo la Chang’ombe na kwa mujibu wa idadi ya mifugo iliyopo tayari imejitosheleza. Mifugo iliyovamia ni zaidi ya 4000 na kwamba ardhi ya kijiji haiwezi kutunza idadi kubwa ya mifugo.

Bw. Said Mmbelwa mwanakijiji wa Chogo kitongoji cha Kibamba aliwaeleza wananchi wenzake kuwa walifanya makosa kuwakaribisha wafugaji hao bila kufuata utaratibu na kwamba kama wananchi weneyewe wasipobadilika basi migogoro ya wakulima na wafugaji haitakwisha.

Aidha Diwani wa kabuki ndani  Mh. Abdallah Pendeza aliwashukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji na Kuwataka wananchi kutekeleza yale ambayo viongozi wamewaelekeza kwa kushirikiana, kwamba kila mmoja atimize wajibu wake kulingana na sheria, taratibu na kanuni.

Mkuu wa Wilaya aliwataka viongozi wa vijiji kuhuisha kamati za ulinzi na usalama na kuhakikisha wanaripoti kwenye vyombo vya sheria pindi wanapoona kunamtu ameingia kwenye maeneo yao haeleweki ili kulinda amani.

Imetolewa na
Alda Sadango
Afisa Habari


Halmashauri ya Wilaya Handeni

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad