Michezo : Yanga yaibamiza Majimaji 3 -0 ,Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


10 Sept 2016

Michezo : Yanga yaibamiza Majimaji 3 -0 ,Jijini Dar


 Beki wa Yanga, Vicent Andrew akiruka juu kuondosha hatari iliyoelekezwa langoni kwao, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.
 Hii ni bambi kwa bambi: hapo ni Donald Ngoma wa Yanga, akichuana vikali na Beki wa Maji Maji, Bahati Yussuf.
 Kiungo wa Yanga, Thaban Kamusoko akiwania mpira na Beki wa Maji Maji, Selemani Kibuta wakati wa Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.
 Kipa wa Timu ya Maji Maji, Aghaton Anthony akiruka kuwania mpira sambamba na Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva na kugongana.
 Kikosi cha Yanga.
 Kikosi cha Maji Maji "Wanalizombe".
 Beki wa Yanga, Juma Abdul akijaribu kuuzuia mpira usitoke nje katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.
 Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva, akionyesha uwezo wa kuuchukua mpira kwa adui yake, wakati wa Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.

 Mshambuliaji wa Yanga, Obren Chirwa, akimtoka beki wa Maji Maji, Ernest Raphael, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.
 Amis Tambwe wa Yanga, akimpiga tobo maridadi, beki wa Maji Maji, Ernest Raphael, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.
 Haji Mwinyi anakwenda na mpira.
 Mwamuzi wa Mchezo huo, Emmanuel Mwandembya akiwaamuru wachezaji wa Maji Maji waache kumzonga baada ya kutoa adhabu ya Penati kufuatia mchezaji wa mmoja kuushika mpira ndani ya 18.
 Hii ni pale mzuka wa kushangilia umekupata, halafu ghafla mwamuzi anaamua kuwa hukuupiga vyema mpira huo na kuamuru kurudiwa.
 Mzozo kidogo kati ya Mwamuzi na Wachezaji wa Yanga.
 Inapigwa tena na inapiga besela na kurudi uwanjani.
 anatokea Deus Kaseke na kutupia tena na kuiandikia Yanga bao la kuongoza dhidi ya Maji Maji.
 
Kipa wa Maji Maji akitafakari baada ya kufungwa.

 Tobo lingine kwa Beki huyu.
 Hii ni bambi kwa bambi: hapo ni Donald Ngoma wa Yanga, akichuana vikali na Beki wa Maji Maji, Bahati Yussuf.
 

 Chenga ya mwili: Mchezaji wa Yanga, Simon Msuva akimkwepa Beki wa Maji Maji, Hamad Kibopile, wakati wa Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara dhidi ya Timu ya Maji Maji ya Songea, uliopigwa jioni ya leo kwenye Uwanja Uhuru, Jijini Dar es salaam. Yanga imeshinda bao 3-0.

 Hapo ni ajali kazini.
 Matokeo baada ya ajali hiyo.










 



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad