Na Freddy Macha : Matukio Mbalimbali Kutoka London Julai 2016 - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


18 Jul 2016

Na Freddy Macha : Matukio Mbalimbali Kutoka London Julai 2016


Picha na habari za Freddy Macha, London Barabara ya Bond jijini London- pic by F Macha 2016 Mwezi Julai Uingereza umekuwa wa vishindo vya kihistoria. Baba yao ni kujitoa Uingereza nje ya Jumuiya ya Ulaya (EU) na kuteuliwa Waziri Mkuu mpya mwanamke, Theresa May. Kwa Watanzania, Uingereza mabadiliko ya mabalozi yalisikika. Jumuiya ya Watanzania na Waingereza (British Tanzania Society) ilimkaribisha rasmi Dk Asha Rose Migiro na mwenzake mpya Tanzania, Bi Sarah Cooke. Bi Cooke aliyekuwa zamani Bangladesh alichukua nafasi ya Bi Dianna Melrose aliyesema aliwapenda sana Watanzania na lugha ya Kiswahili.
Mwezi Julai umeshuhudia fainali za kombe la soka Ulaya (Euro 2016), michuano ya Tennis uwanja maarufu wa Wimbledon na matamasha mbalimbali za fasihi, ambapo mwandishi wa habari hizi alihudhuria kuiwakilisha Tanzania kwa ngoma. Wakati kilio cha ugaidi na mauaji vikitafuna kama chawa, Marekani , Ufaransa na Uturuki, London palifanyika maandamano ya takriban wakazi milioni moja wakipiga kelele maisha magumu na aghali .... 1- Mabalozi wapya Sarah Cooke na Dk Asha Rose Migiro- pic by F Macha 2016Kipya Knyemi, ukumbi wa SOAS, London, 7 Julai. Balozi mpya wa Uingereza,Tanzania Bi Sarah Cooke na Mheshimiwa Dk Asha-Rose Migiro aliyechukua nafasi ya Mhe. Peter Kallaghe. 2 -Bw Yusufu Kashangwa, Mabalozi Sarah Cooke, Dk Migiro na Dianna Melrose-pic by  F Macha 2016Mkurugenzi wa Kituo cha Biashara , Ubalozi Tanzania, London, Bw Yusufu Kashangwa na Balozi Dk Asha Rose Migiro na mabalozi wa Uingereza, Bi Sarah Cooke (wa pili ) na mstaafu Dianna Melrose, ndani ya tafrija hiyo ya BTS, chuo cha lugha SOAS, London. 3-Mandamano ya Jumamosi 16 Julai 2016- picha ya Twitter Maandamano ya wananchi na vyama vya upinzani yaliyofanyika Jumamosi 16 Julai, London , kushutumu hali ngumu na kufunga mkanda (“austerity”) inayozidi kuwadhalilisha maskini na wafanyakazi wa kawaida, Ulaya. Picha ya Twitter 4-Janet Chapman wa BTS akiongea na Adjoa Ajimadu toka Ghana- pic by F MachaJanet Chapman (kulia) mwanaharakati na mwanachama wa BTS ambaye muda mrefu amepigania haki za wasichana na wanawake wanaokeketwa Tanzania akizungumza na Adjoa Ajimadu, toka Ghana katika tafrija hii ya mabalozi wapya SOAS. 5-Tamasha la Mashairi Ledbury, UingerezaBango la tamasha maarufu la kimataifa la Ledbury, Uingereza lililoshirikisha miaka 400 ya maisha ya mwandishi nguli William Shakespeare. Tanzania iliwakilishwa na mwandishi wenu. 6- Bi Hope Katanga akiwa na Bw Julian Marcus na mkewe- pic by F Macha 2016Bi Hope Katanga, Mtanzania na Julian Marcus na mkewe, wanachama waaminifu wa Jumuiya hii ya Waingereza na Watanzania. 7-Dk Andrew Coulson akizungumza na askari wa vita vya pili vya dunia Kapteni David Nichol- pic by F MachaDk Andrew Coulson, (kulia) mhadhiri wa chuo kikuu cha Birmingham, aliyesimamia shughuli ya kuwakaribisha mabalozi. Hapa anazungumza na askari aliyepigana vita vya pili vya dunia, Kapteni David Nichol. Kapteni Nichol aliyewahi pia kuwa mkuu wa mkoa mmoja, Tanganyika enzi za ukoloni , ana umri wa miaka 95 na huitembelea Tanzania mara kwa mara na mkewe. 8-F Macha tamasha la Fasihi ya Wabangladesh London 2016Mwandishi na mwanamuziki Freddy Macha baada ya kutumbuiza ngoma tamasha la fasihi la Wabangladesh, London.  


Balozi Dk Asha- Rose Migiro akisalimiana na Bw Alistair Scott wa kampuni ya mafuta ya Ophir Energy inayotazamia kujihusisha kikamilifu na madini hayo Tanzania. Wataalamu kadhaa wa Ophir Energy walihudhuria hafla hii ya SOAS.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad