Muziki : BASATA Imemfungia Snura Kujihusisha na masuala ya Sanaa , pamoja na Video yake ya CHURA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


4 May 2016

Muziki : BASATA Imemfungia Snura Kujihusisha na masuala ya Sanaa , pamoja na Video yake ya CHURA



Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza rasmi kumfungia msanii wa bongo fleva Snura kujihusisha na masuala ya sanaa. Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Zawadi Msalla ameongea na waandishi wa habari na kuthibitisha taarifa hizi.
Wimbo huu wa Chura umefungiwa kutochezwa kwenye redio na TV nchini. Taarifa hiyo imetolewa na wizara hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wake wa mikutano wizarani hapo  Dar es salaam.
Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo ,Zawadi Msalla, pia imewaonya watu kutoisambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo whatsApp, amedai kwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad