Matukio : TRA yafungua mafunzo ya awamu ya pili kwa wafanyakazi wake. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


18 May 2016

Matukio : TRA yafungua mafunzo ya awamu ya pili kwa wafanyakazi wake.


 Mkuu wa chuo cha Kodi (TRA), Profesa Isaya Jairo  akizungumza  wakati wa hafla kufungua mafunzo ya awamu yapili ya wafanyakazi wa mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) Amesema kuwa wameamua kuanzisha mpango huo kwa kushirikiana na Mamlaka ya mapato  ili kufundisha wafanyakazi wa TRA maadili na nyenzo za utendaji kazini  pamoja na kuendesha mafunzo ya dini ili kuwafanya wafanyakazi wawe wacha Mungu katika kazi zao.
 Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa TRA, Victor Kimaro akizungumza na wafanyakazi wa malaka ya Mapato Tanzania(TRA) wakati  wa kufungua mafunzo ya awamu ya pili kwa wafanyakazi wake 200. Pia amewataka wafanyakazi wote wanatakiwa wafanye kazi kwa maadili hususani upande wa ukusanyaji kodi na Chuo hicho kimewafundisha wafanyakazi hao kufanya kazi kwa ushindani katika maeneo ya kazi ili kuliletea taifa maendeleo yaliyokusudiwa.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Dar es Salaam leo. wakati wa kufungua mafunzo ya maadili kwa wafanyakazi wa TRA ambao wamefanya usaili na kufanikiwa kufunzu kusoma mafunzo hayo kwa wafanyakazi kwaajili ya kujifunza mambo mtambuka ya tasinia ya TRA. Lengo la kuwapa mafunzo hayo ni kutaka kuijenga Mamlaka ya Mapato (TRA) mpya.Kulia ni Mkuu wa chuo cha Kodi (TRA), Isaya Jairo na Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasiliamali watu na utawala katika chuo cha Kodi(TRA), Victor Kimaro wakiwa katika mkutano wa kufungua mafunzo ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA).
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata  akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA)leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata na  Mkuu wa chuo cha Kodi (TRA), Profesa Isaya Jairo wakikata utepe kuzindua ripoti ya mafunzo kwa wanafunzi wa malaka ya Mapato Tanzania jijini Dar es Salaam leo.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata (Katikati walioshika vitabu ),Mkuu wa chuo cha Kodi (TRA), Profesa Isaya Jairo(Kulia) na Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa TRA, Victor Kimaro (kushoto) wakionyesha vitabu vya mafunzo kwa wafanyakazi wa TRA jijini Dar es Salaam leo.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata  akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TRA jijini Dar es Salaam leo. Wafanyakazi hao ndio wanaohudhulia mafunzo hayo.
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata  amesema kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) imebakiza Tsh. Trilioni 2.363 ili kufikia lengo  walilojiwekea la kukusanya mapato ya trilioni 12.363 katika  mwaka wa fedha 2015/16, ambapo hadi sasa imekusanya kiasi cha Tsh. Trilioni 10. Ameyasema hayo wakati wa  hafla ya uzinduzi  wa awamu ya pili ya mpango wa mafunzo kwa wafanyakazi waliopo kwenye fursa ya ajira za taasisi hiyo.
Mkuu wa chuo cha Kodi (TRA), Profesa Isaya Jairo.
Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa TRA, Victor Kimaro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad