Kimataifa : Mtanzania Freddy Macha na ngoma ya wasifu wa gwiji William Shakespeare - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


14 May 2016

Kimataifa : Mtanzania Freddy Macha na ngoma ya wasifu wa gwiji William Shakespeare


Watanzania walikuwa miongoni mwa washindi wa tuzo la kudumisha utamaduni na maisha ya Mwafrika Ughaibuni.  Hamida Mbaga ( wa tatu kulia) anayeendesha biashara ya mavazi, Manchester na Freddy Macha – tuzo la kuendeleza muziki na utamaduni. Kati kati ni mchoraji na mbunifu mavazi Jasmine Kissamo./PICHA NA MAKTABA

Tarehe 23 April, 2016.... ilitimia miaka 400 tangu gwiji wa fasihi, mashairi na tamthiliya, mwandishi maarufu wa Kiingereza, William Shakespeare alipofariki. Mwasisi wa taifa la Tanzania ,Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kutafsiri Kiswahili  kazi mbili za Shakespeare :” Mabepari wa Venice” (Merchants of Venice) na “ Julius Kaizari” (Julius Caesar) ...
Wasanii mbalimbali  duniani wamekuwa wakijumuika kutukuza kazi za nguli huyu asiyechuja kwa visa, lugha, nahau, misemo na mada za kila namna. Miongoni mwao ni kundi maalum - “Bards without Borders” (Watenzi Wasio na Mipaka), jijini London.  Ndani  wamo washairi  wa Somalia, Nigeria, Bangladesh, Zimbabwe, Jordan, Colombia, Afghanistan,  Bosnia, Ujerumani, Jamaica, Uingereza, India na Tanzania. Mwakilishi wa Tanzania ni mwandishi  Freddy Macha.  Anatumia muziki wa ala mbalimbali ikiwemo Ngoma kumnadi Shakespeare.
Wakati  maonesho mbalimbali yakiendelea kwa kasi Uingereza, Macha ametafsiri kazi zake Shakespeare kwa Kiswahili na pia kuandika tenzi mpya na kikundi hiki. Moja ya tukio lililofanyika April 23 ,  klabu mashuhuri ya Rich Mix, London mashariki,  Macha alichanganya mapigo ya Ngoma kadhaa za  Kiafrika ikiwepo Sindimba ya Tanzania kutambika na kumsifia gwiji William Shakespeare.
VIDEO
HABARI ZAIDI

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad