Matukio : Mhe. Samia Suluhu afungua Kongamano la wanawake katika uongozi , Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Wednesday, 13 April 2016

demo-image

Matukio : Mhe. Samia Suluhu afungua Kongamano la wanawake katika uongozi , Jijini Dar


1
 Makamu wa Rais Samia Hassan Suluhu akihutubia wakati akifungua kongamano la wanawake katika uongozi lililofanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo asubuhi. Kongamano hilo liliandaliwa na Taasisi ya Uongozi.
2
 Taswira ya meza kuu katika kongamano hilo.
3
  Makamu wa Rais Samia Hassan Suluhu (kushoto) na Spika wa Bunge mstaafu wakiwa kwenye kongamano hilo.
4
 Mwanasheria Vicky Mandali akichangia jambo kwenye kongamano hilo.

6
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Wanawake Tanzania, Mary Lusindi akitoa mchango wake katika kongamano hilo.
IMG_0958
 Balozi Mwanaidi Maajar, akichangia jambo kwenye kongamano la wanawake katika uongozi lililofunguliwa na Makamu wa Rais Samia Hassan Suluhu. Kongamano hilo liliandaliwa na Taasisi ya Uongozi.
IMG_0961
 Wadau  wakiwa kwenye kongamano hilo lililowajumuisha wanawake wenye taaluma mbalimbali na viongozi.
IMG_0964
 Kongamano likiendelea.
IMG_0965
 Taswira kwenye kongamano hilo.
IMG_0978
Usikivu wa mada kwenye kongamano hilo.

Na Dotto Mwaibale

VIONGOZI mbalimbali nchini wametakiwa kutumia uwezo na nyazifa zao ili kuwahamasisha na kuwawezesha wanawake wapate maendeleo.

Mwito huo umetolewa na Makamu wa Rais Samia Hassan Suluhu wakati akifungua kongamano la wanawake katika uongozi lilifanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo asubuhi ambalo liliandaliwa na Taasisi ya Uongozi.

"Kila mtu na hasa sisi viongozi katika uwezo wetu na nyadhifa zetu tuzingatie kutumia kila nafasi kwenye ofisi zetu kuwahamasisha na kuwawezesha wanawake" alisema Suluhu.

Suluhu alisema wanawake wanapaswa kupewa sauti katika maamuzi mbalimbali na kama tunavyosema ukimuelimisha mwanamke unakuwa umeelimisha taifa zima.

Alisema usemi huo wa wahenga ukaonekane katika ushiriki wao na aina ya maamuzi watakayoyafanya na kuyasimamia ili yalete tija kwao na taifa kwa ujumla.

Samia alisema kwamba kongamano hilo lenye maudhui ya wanawake katika uongozi lina lengo la kuwapatia nafasi wanawake ambao wako kwenye uongozi na wale wanaokusudia kuwa viongozi katika maeneo mbalimbali ikiwemo serikali, kwenye vyama vya soasa, sekta binafsi, vyama visivyo vya kiserikali, kushirikiana katika kutambua mazingira wezeshi katika kumpatia mwanamke fursa ya kufikia nafasi ya uongozi.

Alisema Tanzania uwakilishi wa wanawake ndani ya chombo cha uwakilishi na maamuzi ambacho ni Bunge ni asilimia 30 lakini wamejiwekea lengo la kufikisha asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *