Teknolojia : Mshindi wa shindano la Teknolojia kupatikana leo - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


31 Mar 2016

Teknolojia : Mshindi wa shindano la Teknolojia kupatikana leo


Mshindi wa shindano la uvumbuzi wa Teknolojia mpya itakayo saidia jamii kupatikana leo na kuzawadiwa shilingi milioni tano (5,000,000) katika mkutano wa wadau wa teknologia unaofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkutano huo umeandaliwa na Bites&Bytes ukishirikiana na IBM, TWAWEZA, FSDT pamoja na CBA, mktano huo ambao utahamasisha uendelezaji wa mawazo mapya na uvumbuzi kwa waanzishaji wapya wa biashara na kuwapa mwanya wa kubadilisha mawazo na wadau wengine.




Mwanzilishi wa Bits&Bites, Lilian Madeje akiwakalibisha wageni na kufungua mkutano wa Uvumbuzi wa Teknologia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa mwalimu Nyerere.
Mwakilishi wa IBM na mstakabali wa Innovation, Ben Mann akifafanua jinsi IBM ilivyofanya kazi kwenye Teknologia hapa nchini.
 Mwakilishi mwenza wa Bits&Bytes,Zuweina Farah akizungumza na wadau wa Teknologia waliokusanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.


Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya DTREE, Lucy Silas akizungumza na wadau wa teknolojia na uvumbuzi wa teknologia katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.
  Baadhi ya wadau wa Teknologia wakimsikiliza  mtoa mada (Hayupo) pichani jijini Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere.
  Mwakilishi mwenza wa Bits&Bytes,Zuweina Farah akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Teknologia na uvumbuzi wa teknologia mpya itakayo wasaidia wanachini kufanya kazi kwa urahisi zaidi, leo katika ukumbi wa mikutano wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo.
Amesema kuwa leo washiriki 16 walioshiriki kuvumbua teknoloia mpya wameshiriki katika mkutano huo na ndipo mshindi atakaye fanikiwa kushinda katika shindano hilo atazawadiwa shilingi Milioni 5 kwa kuwa na wazo zuri kuliko wengine ili aweze kuwa na mtaji kwaajili ya kuendeleza uvumbuzi wake.
Mwanafunzi mshiriki wa uvumbuzi wa Teknologia mpya itakayo wasaidia jamii, Gibson Kawago wa shule ya Sekondari ya huko Arusha akiwa amegundua taa za miale ya jua(Solar Power) zinazoweza kuchaji simu za Smati kwa zaidi ya masaa nane.
 Mwakilishi wa Fist Financial Sector Deeping(FSDT), Revis Mushi akizungumza na waaandishi wa habari katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa mkutano huo utasaidia jamii na wananchi kwa ujumla kusaidia kupata mfumo mwepesi wa Teknologia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Atamizi (DTB) ambayo ipo tume ya Sayansi, George Mulamula akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere kuhusiana na amesema kuwa Tume ya Sayansi imeungana katika mkutano wa Teknologia ili kuwapa ujuzi zaidi Vijana. Pia amesema kuwa katika Tume ya Sayansi wameweza kuvumbua mfumo wa Max Malipo na wa mfumo wa kudahili wanafunzi wa TCU.
Mshiriki na Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jangwani,  Necta Richard akizungumza na waandishi wa habari leo mara baada ya mkutano wa Teknologia uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. 
Baadhi ya washiriki katika mkutano wa Teknologia. 


 Washiriki.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad