Michezo : Ujenzi wa uwanja wa Kaitaba Kumalizika Mapema Mwaka huu - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


13 Feb 2016

Michezo : Ujenzi wa uwanja wa Kaitaba Kumalizika Mapema Mwaka huu



Junior Mwemezi wa Azam Tv na Faustine Ruta
Magari yaliyowasili hii leo katika Uwanja wa Kaitaba yaliyoleta vifaa kwa ajili ya Umaliziaji wa Ujenzi wa Uwanja ambao ujenzi wake ulikuwa ukisua sua kutokana na kukwama kwa Vifaa hivyo Jijini Dar es salaam.



Mesh rubber crumb




Mshauri wa ufundi Bwana Rutayunga Peregrinus akiteta jambo na waandishi wa habari(kulia) leo kwenye Uwanja wa Kaitaba juu ya Umaliziaji wa Uwanja huo muda mfupi baada ya Vifaa hivyo kuwasili hii leo. Picha Na Faustine Ruta wa bukobasports.com

Mshauri wa ufundi Bwana Rutayunga Peregrinus

Ndipo akafafanua kwamba Uwanja baada ya Vifaa kuwasili umaliziaji utaanza mara moja huku akisisitiza kwamba Mwezi huu wa februari kama mambo yaenda vyema utamalizika. Na Timu ya Kagera Sugar itamalizia michezo yake ya Msimu huu kwenye Uwanja huu. Pia Bukobasports imeweza kupata habari zaidi kuwa Rais wa TFF Bw. Jamal Malinzi nae yupo Mjini hapa Bukoba akifuatilia Mradi huo wa Uwanja unavyoendelea na kesho Jumamosi atakutana na Viongozi wengine na kuteta nao na hatimae kukamilisha Ujenzi huo wa Uwanja Mwezi huu wa Februari.

Afisa utamaduni wa Mkoa wa Kagera Bw. Rugeiyamu nae alikuwepo katika Uwanja huo. Picha Na Faustine Ruta wa bukobasports.com

Junior Mwemezi wa Azam Tv akiteta jambo na Mshauri wa ufundi Bwana Rutayunga Peregrinus

Swala zima ni juu ya Umaliziaji wa Uwanja wa Kaitaba ndicho kilichokuwa kikisisitizwa leo baada ya Vifaa kuwasili.

Sehemu ya Uwanja huo kama unavyoonekana ukiwa ulishawekwa nyasi bandia

Sehemu ya Ukingo ambayo ukutanisha maji na kuyatoa nje kupitia kwenye bomba maalum.Junior Mwemezi wa Azam Tv na Fausti Ruta Taswira ya Uwanja wa Kaitaba ulivyo kwa sasa.Junior Mwemezi wa Azam Tv na Fausti Ruta wa bukobasports walipata muda wakapumzika japo kwa uchache katika Uwanja huo ambao unaelekea kumalizika ujenzi wake.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad