Matukio: Naibu waziri azitaka Mamlaka za kutatua kero za Mipakani - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


1 Feb 2016

Matukio: Naibu waziri azitaka Mamlaka za kutatua kero za Mipakani





Na Ferdinand Shayo wa Wazalendo 25 Blog,Arusha.

Naibu Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa  Afrika Mashariki Susan Kolimba amezitaka mamlaka zinazofanya kazi katika mpaka kati ya Kenya na Tanzania wa Holili kuhakikisha kuwa wanatatua matatizo ya uchache wa wafanyakazi,uhaba wa vitendea kazi ili kuhakikisha kuwa wanatatua kero za wananchi wanaofanya biashara na shughuli za kijamii katika ukanda wa Afrika mashariki.

Akizungumza mara baada ya kufanya ziara yake mwishoni mwa wiki katika mpaka wa Holili ambapo alizungumza na wafanyakazi wa vitengo mbali mbali vya serikali ikiwemo TBS,TFDA,Uhamiaji,Polisi pamoja na idara nyingine ambazo ziliwasilisha changamoto zao mbele ya waziri huyo ambaye aliahidi kuzifikisha kwa mamlaka husika ili ziweze kutatuliwa.

“Tunahitaji kuboresha huduma katika mipaka ili biashara zienfdelee na kukuza mahusiano mazuri katika jumuiya ya Afrika mashariki “ Alisema Kolimba

Mkaguzi wa TFDA ,Edward Mwamilawa amesema kuwa licha ya unyeti wa mpaka huo bado ofisi yake inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya kitaalamu vya kupima ubora wa vyakula na vipodozi jambo ambalo linazorotesha utendaji hivyo ameiomba serikali isaidie kitengo hicho ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Mkuu wa kituo cha TRA mpaka wa Holili Mwaikalobo Aden na Afisa wa Mamlaka ya Kukusanya kodi nchini Kenya (KRA) Dan Nyambaka wamesema kuwa ukusanyaji wa mapato katika mpaka huo umekua ukiongezeka kutokana na biashara inayofanyika kati ya Tanzania na Kenya .

Kuanzishwa kwa kituo kimoja Mpakani (One Stop Border Post) kimerahisisha upatikanaji wa huduma za kiutawala na kurahisisha biashara kati ya nchi Mwanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki  .

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad