Matukio /Maisha : Mtandao wa Wanawake Wahitimisha Tamasha la Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi, Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


6 Sept 2015

Matukio /Maisha : Mtandao wa Wanawake Wahitimisha Tamasha la Uzinduzi wa Ilani ya Uchaguzi, Jijini Dar

 Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akizungumza na wananchi juu ya kutambua michango ya kimaendeleo inayofanywa na wanawake kwa kuwawekea kumbukumbu kama ilivyo kwa wanaume, ili kuleta uwiano wa kijinsia leo Jiji Dar es Salaam katika kilele cha tamasha la Jinsia.
 Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akiteta jambo na Ruth Meena.
 Wanawake wakitaja baadhi ya matatizo ambayo yanayowakabili ni pamaoja na suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama maeneo mbalimbali nchini.
Wanawake wameitaka tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) kutofumbia macho suala la matusi na kejeli zinazofanywa na viongozi wa siasa katika kampeni zao.
 Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Lilian Liundi akiwa katika picha ya pamoja na wa mama walioshiriki maadhimisho hayo leo jijini Dar es Salaam
Sehemu ya wananchi waliofika katika maadhimisho hayo jijini Dar es Salaam (Picha na Emmanuel Massaka).
WATANZANIA wametakiwa kuchagua viongozi ambao sera ya ilani ya vyama vyao, itatatua kero zao na iwe yenye kutekelezeka kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa na sio ya kibinafsi.
Wakiwakisilisha maadhimio mbalimbali katika kilele cha Tamasha la Jinsia jijini Dar es Salaam, wananchi kutoka warsha mbalimbali, wamesema kuwa watanzania wametakiwa kuwa makini kwa kuwachagua viongozi ambao watawahaidi sera zinazo tekelezeka na sio vinginevyo.
Wakitaja baadhi ya matatizo ambayo yanawakabili ni pamaoja na suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama maeneo mbalimbali nchini, hivyo watahakikisha wanawauliza wagombea wa ngazi mbalimbali za uongozi ikiwemo udiwani, ubunge na urais, ni kwa kiasi gani watashughulikia suala la huduma ya maji.
Vilevile wamesema chama kitakacho pata ridhaa ya kuiongoza Tanzania kwa awamu ya tano, ifanye mabadiliko ya katiba ambayo yataondoa mfumo kandamizi dhidi ya mwanamke, pia wameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutofumbia macho suala la matusi na kejeli zinazofanywa na viongozi wa siasa katika kampeni zao, jambo ambalo linaweza chochea uvunjifu wa amani nchini, huku wakiwataka tume kutenda haki kwa vyama vyote vinavyo shiriki katika uchaguzi mkuu.
Hivyo wameitaka serikali kutambua michango ya kimaendeleo inayofanywa na iliyofanywa na wanawake kwa kuwawekea kumbukumbu kama ilivyo kwa wanaume, ili kuleta uwiano wa kijinsia, pia wamesema watahakikisha wanaishauri serikali kuandaa sera maalumu itakayo tambua mchango wa wanawake na kuweka kumbukumbu katika makumbusho maalum ya wanawake.
Huku wakiwataka waandishi wa habari kutumia taaluma yao kwa kutoa elimu ya uraia na masuala mbalimbali mtambuka yenye tija kwa maendeleo ya ukombozi wa taifa.
Tamasha hilo la kijinsia lililo andaliwa na wadau mbalimbali wa masuala ya kijinsia kwa kushirikiana na mtandao wa kijinsia TGNP, limefikia kilele leo jijini Dar es Salaam likibeba kauli mbiu ya mifumo kandamizi ya Mageuzi ya mifumo kandamizi hayaepukiki.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad