Matukio : Vijana Wahamasishana juu ya Fursa Zilizopo ndani na nje ya Nchi - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Aug 2015

Matukio : Vijana Wahamasishana juu ya Fursa Zilizopo ndani na nje ya Nchi

Mwenyekiti na mwanzilishi wa kikundi cha vijana cha Tanzania Youth Network (TYN), Agnes Mgongo akizungumza na vijana mara baada ya kukutana  katika ukumbi wa Don Bosco  jijini Dar es Salaam.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda akizungumza na vijana mbalimbali waliounda kikundi kiitwacho Tanzania Youth Network (TYN), wakijadili changamoto mbalimbali zinazowakumba vijana pamoja na vijana kuunda vikundi mbalimbali ili kutumia fursa zilizopo hapa nchini na Nje ya nchi ameyasema hayo katika mkutano uliowakutanisha vijana hao katika ukumbi wa Don bosco jijini Dar es Salaam.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda  akipokea kitabu cha ujasiliamali  kutoka kwa Balozi wa vijana wa jumuia ya Afrika Mashariki, Eric Ngilangwa katika mkutano wa vijana uliofanyika jijini Dar es Salaam.

 Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda, Mwenyekiti na mwanzilishi wa kikundi cha vijana cha Tanzania Youth Network (TYN), Agnes Mgongo na Katibu wa TYN, Azavery Phares wakiwa katika mkutano wa vijana uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya vijana wakiwa katika mkutano uliowakutanisha vijana mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Afisa vijana  wa wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo, Racheal Kasanda akiwa katika picha ya pamoja na kikundi kilichowakusanya vijana mbalimbali kutoka Bagamoyo,Morogoro pamoja na Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad