Awali
ya yote nirudie kutoa pongezi kwa serikali kwa hatua hii muhimu waliyofikia ya
kuwasilisha mswada wa sheria mtandao ambao naimani kubwa itakua na majibu
mazuri ya kudhibiti na kuhimili vishindo vya uhalifu mtandao nchini. Naomba
itambulike Tanznaia si ya kwanza kuwa na sheria za usalama mitandao na ukweli
ni kwamba tumechelewa kwa kiasi Fulani. Nchi nyingi tayari zinasheria za
usalama mitandao na zimeendelea kuboreshwa kadri teknolojia inavyo endelea
kukua na kubadilika.
Nitaanza
na mifano michache kunasheria mitandao zilizopendekeza kifungo cha maisha kwa
wahalifu mtandao nchini Uingereza. Na katika Kikao cha usalama mitandao
kilichopita mshiriki aliyekua nami meza kuu katika kuongoza moja ya kikao
aliyetokea “US Secret service” alipata kuainisha adhabu ya miaka kumi na sita
bado imeonekana ni ndogo na inashauriwa kuongezwa makali.
Aidha,
Nieleze ushauri wa kuhakiki sheria mitandao zinaboreshwa na kuwa kali zaidi ni
kutokana na athari ya uhalifu mtandao kua kubwa sana na imekua ikimgusa kila
mmoja wetu – Kwan nje ya nchi kila siku tumekua tukipata habari mpya ya matukio
ya kiuhalifu mtandao ambapo maelfu wamekua wakipoteza maisha, fedha na pia
ufaragha wao umekua ukitumiwa vibaya na wahalifu mtandao.
Tanzania
pia hatuko salama – Nimekua nikipata malalamiko mengi ya watu kudukuliwa
faragha zao, kuibiwa fedha nyingi sana na wengine kufikia hata kujitoa maisha
kwa kudalilisha mitandaoni.
Hayo
yote yamekua yakisukuma wataalam usalama mitandao kuumiza vichwa kuhakiki
wanakuja na mwarubaini wa uhalifu huu mtandao unaozidi kuota mbawa kila
kukicha. Hapo ndipo mengi yakawekwa sawa katika kukabiliana na hali hii ikiwa
ni pamoja na kukuza uelewa kwa watumiaji mtandao (Matumizi salama ya mitandao),
Kuzalisha na kuongezea uwezo kwa wataalam wa usalama mitandao, kuwa na sharia stahiki
za uhalifu mitandao, kukuza ushirikiano kutokana na uhalifu huu kutokua na
mipaka, kuhimiza kupatikana kwa takwimu sahihi za uhalifu mitandao ili kuweza
kutambua maeneo athirika zaidi.
Kwenye
hili la Sheria ni hatua nzuri sana ambapo Tanzania imefikia ili kuweza kurahisisha
mapambano dhidi ya uhalifu mtandao nchini na kuhakiki taifa linabaki salama
kimtandao. Naimani Kila mmoja wetu ukizingatia wote ni wahanga kwa namna moja
au nyingine ya uhalifu mtandao lazima tufurahie na kulipokea hili kwa mikono
miwili. Wataalam wa usalama mitandao wamefurahishwa sana na hatua hii yetu na
pongezi ni nyingi sana hadi sasa.
Kuondoa
hofu Watanzania naomba nieleze kwamba katika kuandaa muswada huu wataalam na
wadau mbali mbali walishirikishwa na badae kuvuka mipaka kwa wataalam kutoka
mataifa mbali mbali katika maswala haya ya usalama mitandao kutoa maoni yao na
kuboresha – Haikukomea hapo imepitia hatua kadhaa na hata kupelekea kauli yangu
niliyo itoa katika moja ya vikao vya wataalam wa usalama mitandao kueleza kuwa “
Hatua za kitaalam zimekwisha sasa ipo kwenye hatua za kisiasa kuweza kupatiwa Baraka
kabla ya kuwasilishwa bungeni” – Kauli ambayo wataalam
Nimepata
kufatilia kwa karibu kinachozungumzwa na wengi, Hofu kubwa nilizo ziona ambazo
nimeona nizitole ufafanuzi ni kama ifuatavyo: -
MOJA,
hofu kuwa uchunguzi wa makosa haya inaweza ikawa inakiuka faragha. Naomba nieleze
kuna anaefahamu faragha yake iko dhaifu kiasi gani mara tu anavyo kua
mtandaoni? Ni wazi kabisa unapaswa kujua faragha haiingi matatani tu kwa sababu
ya sharia hizi mtandao.
Uchunguzi
wowote wa uhalifu mitandao duniani kote unahusisha uangalizi wa kina hatua kwa
hatua kwa kila ushaidi wa kielektroniki ikiwa ni pamoja na kupitia kwa karibu
kila chembe ya shaka ya kile kinachoweza kuonekana kinaweza kuwa na chembe ya
sababu ya uhalifu mtandao.
KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA >>>
No comments:
Post a Comment