Habari : Dk. Gharib Bilal Akutana na Uongozi wa Kampuni ya Mwananchi Communication - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Friday, 13 February 2015

demo-image

Habari : Dk. Gharib Bilal Akutana na Uongozi wa Kampuni ya Mwananchi Communication

01
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communication, Francis Nanai,  wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Feb 13, 2015 kwa mazungumzo na kujitambulisha rasmi baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo. Kushoto ni Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bakari Machumu.
02
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Uongozi wa juu wa Kampuni ya Mwananchi Communication, Mkurugenzi Mtendaji Francis Nanai  (katikati) na Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bakari Machumu,  wakati walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo na kujitambulisha rasmi baada ya kuteuliwa kushika nafasi hiyo na kuelezea kazi zinazofanywa na kampuni hiyo. 
001
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Uongozi wa juu wa Kampuni ya Mwananchi Communication, Mkurugenzi Mtendaji Francis Nanai  (kulia kwa Makamu), Mhariri Mtendaji wa Kampuni hiyo, Bakari Machumu, na Mshauri wa Kampuni hiyo, Teddy Mapunda wakati walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo kwa mazungumzo na kuelezea kazi zinazofanywa na kampuni hiyo. 
004
Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa juu wa Kampuni ya Mwananchi Communication, Mkurugenzi Mtendaji Francis Nanai  (wa pili kushoto) Mhariri Mtendaji Bakari Machumu (kulia) na Mshauri wa Kampuni hiyo, Teddy Mapunda (kushoto) baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *