TUWATUMIKIE WANANCHI :RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA KISIMA CHA MAJI, LAMBO KATIKA KIJIJI CHA JAMII YA WAFUGAJI CHA MBALA,CHALINZE - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Monday, 11 August 2014

demo-image

TUWATUMIKIE WANANCHI :RIDHIWANI KIKWETE AZINDUA KISIMA CHA MAJI, LAMBO KATIKA KIJIJI CHA JAMII YA WAFUGAJI CHA MBALA,CHALINZE


01
 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete akionozana na akina mama wa jamii ya kimasai waliobeba maji waliyoyateka baada ya mbunge huyo kuzindua kisima cha maji katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, Bagamoyo mkoani Pwani jana. Kisima hicho pamoja na lambo la kunyweshea mifugo vimejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. Kushoto ni Kiongozi wa mradi huo, Joseph Chagama na nyuma yake ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana.
IMG_0667
 Ridhiwani Kikwete akifunua pazia ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kisima hicho. Kushoto ni Askofu wa Kanisa la Wasabato Jimbo la Mashariki,Mark Malekana.
IMG_0673
 Ridhiwani akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa akina mama wa jamii ya kimasai baada ya kuzindua kisima hicho.
IMG_0694
 Ridhiwani Kikwete akifungua maji ikiwa ni ishara ya kuzindua lambo la kunyweshea mifugo katika Kijiji cha Mbala kinachokaliwa kwa asilimia kubwa na jamii ya wafugaji
IMG_0699
 Ng'ombe wakitoka kunywa maji kwenye lambo hilo
IMG_0704
 Watoto wa kimasai waonja maji ya kwenye lambo baada ya uzinduzi
IMG_0712
 Kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Wasabato la Mbala, ikitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa kisima cha maji uliofanywa na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, katika Kijiji cha Mbala, Chalinze, mkoani Pwani jana. Kanisa hilo limejengwa na Kanisa la Wasabato kwa gharama ya sh. mil. 76. 
IMG_0715
 Ridhiwani Kikwete (wa pili kulia) akishiriki katika maombezi
IMG_0719
Kwaya ya Kanisa la Wasabato la Manzese wakimwimbia bwana wakati wa hafla hiyo. . PICHA NA RICHARD MWAIKENDA

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *