MAZISHI YA MZEE SMALL : RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA MCHEZA FILAMU MAREHEMU SAIDI NGAMBA "MZEE SMALL" TABATA ,DAR ES SALAAM - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Tuesday 10 June 2014

MAZISHI YA MZEE SMALL : RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AHUDHURIA MAZISHI YA MCHEZA FILAMU MAREHEMU SAIDI NGAMBA "MZEE SMALL" TABATA ,DAR ES SALAAM

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili kwenye Msiba wa msiba wa msanii maarufu wa filamu ya vichekesho hapa nchini,Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam  Juni 9, 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwafariji wafiwa wakati walipokwenda kuhani msiba wa msanii maarufu wa filamu vichekesho Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014
Mama Salma Kikwete akimpa pole mjane wa Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Smal” wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii huyo maarufu wa filamu za vichekesho nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam Juni 9, 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amejumuika na waombolezaji mbali mbali kwenye Msiba wa msanii maarufu wa filamu za vichekesho nyumbani kwa marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam Juni 9, 2014.
Rais Kikwete akisaini Kitabu cha Maombolezo.
Dua zikiendelea kusomwa kumuombea Marehemu Said Ngamba "Mzee Small". 
 MC Mkwere akiongoza shughuli ya Msiba huo.
Waombolezaji Msibani.
 
 Mtoto wa Marehemu Mzee Small,Mahmoud Said Ngamba akionekana ni mwenye Majonzi sana.
 Mmoja kati ya watu waliofanya kazi nyingi na Marehemu Mzee Small,Bwana Tupatupa akiongea na vyombo vya habari.
 Rais Kikwete akiwaaga waombolezaji msibani hapo.

Mama Salma Kikwete akiondoka msibani hapo baada ya Kuhani msiba huo.
Othman Michuzi wa Mtaa kwa Mtaa akiwa na waombolezaji
 Waombolezaji msibani.
 Jeneza likipakiwa kwenye gari tayari kwa safari ya Mazikoni.
 Msafara wa magari na waendesha Bodaboda wakiwa katika barabara ya Segerea Kinyerezi wakati wakielekea Makaburi ya Segerea kwaajili ya Kumpumzisha Kwa Amani Mkongwe wa Sanaa ya Vichekesho Nchini Said Ngamba almaarufu Mzee Small
 Gari lililobeba Mwili wa Marehemu Said Ngamba aka Mzee Small (la kwanza) likiwa limesimama kwaajili ya Vijana kuubeba Mwili wake hadi kwenye Makaburi ya Segerea jioni Hii
 Vijana wakishusha jeneza lenye mwili wa Marehemu Mzee Small kwaajili ya kuelekea kwenye Makaburi ya Segerea
 
Vijana wakiwa wamepanga mstari kuanzia Barabara ya Segerea Kinyerezi hadi makaburini kwaajili ya kupokea jeneza lenye Mwili wa Marehemu Mzee Small
 Watu mbalimbali wakisubiri Mwili wa Marehemu kuwasili katika makaburi ya Segerea
 Mwili wa Marehemu Mzee Small ukitolewa kwenye jeneza tayari kupumzishwa katika Nyumba yake ya Milele katika makaburi ya Segerea.
 Watu mbalimbali wakiwasili kwenye makaburi ya Segerea kwaajili ya kumzika Mzee Small. Picha Zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog

No comments:

Post a Comment