MATATIZO NDANI YA UVUVI :BALOZI IDDI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIVUNGE NA TUMBATU KUHUSU MATATIZO YA UVUVI - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Friday 6 June 2014

MATATIZO NDANI YA UVUVI :BALOZI IDDI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIVUNGE NA TUMBATU KUHUSU MATATIZO YA UVUVI


 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kivunge kuhusu hitilafu za uvuvi kati ya Kijiji hicho na Tumbatu katika uwanja wa michezo wa Good Hope Mkwajuni Mkoa wa Kaskazini Unaguja. Kushoto ya Balozi Seif ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Nd. Haji Juma haji na Katibu wa mkoa Huo Bibi Caterina.
 Umati wa wananchi wa Kivunge wakisikiliza nasaha za Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif hayupo pichani kwenye mkutano wa kutathmini hitilafu iliyojitokeza ya uvuvi kati ya wananachi wa Kivunge na Tumbatu.
 Mwakilishi wa Wananchi wa Kijiji cha Kivunge Bwana Sharifu Kombo Sharifuakitoa Taarifa ya tukio la kuchomwa moto kwa chombo cha Uvuvi cha wavuvi wa Kijiji hicho Kisiwani Tumbatu Mapema Mwaka huu.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Nd. Haji Juma Haji akiwaasa wananchi wa Kivunge kujiepusha na cheche zinazopenyezwa na baadhi ya watu kwenye migogoro yao ya kijamii hapo uwanja wa michezo wa Good Hope Mkwajuni. Picha na Hassan Issa wa – OPMR – ZNZ.

No comments:

Post a Comment