KESI YA MAUAJI :KESI YA MAUAJI NMB MWANGA: WAKENYA KUNYONGWA; MTANZANIA MIAKA 5 JELA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


13 Jun 2014

KESI YA MAUAJI :KESI YA MAUAJI NMB MWANGA: WAKENYA KUNYONGWA; MTANZANIA MIAKA 5 JELA


MAHAKAMA kuu kanda ya Moshi imewahukumu Raia wawili wa Kenya, Samweli Saitoti (Saimoo) na Michael Kimani (Mike), wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), PC Michael Milanzi mwaka 2007.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji mfawidhi wa mahakama kuu, Jaji Kakusulo Sambo alisema baada ya kusikiliza na kutafakari ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo na mashahidi 18 wa upande wa Jamhuri, imeridhika kuwa Jamhuri ilifanikiwa bila kujenga kesi dhidi ya washitakiwa wote watatu bila kuacha shaka lolote.

Raia hao ambao walipambana na polisi jijini Arusha kwa saa sita wakijihami kwa silaha za kivita yakiwamo mabomu ya kurusha kwa mkono na bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG), walifanya mauaji hayo yaliyoambatana na uporaji wa Sh239 milioni mali ya Benki ya NMB, Julai 11, 2007.
Pia, Jaji Kakusulo Sambo wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, amemhukumu Mtanzania, Calist Kanje kwenda jela miaka mitano kwa kuwasaidia wauaji hao wasikamatwe na polisi baada ya kufanya mauaji.
Akitoa hukumu hiyo jana, Jaji Sambo alisema upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Ladslaus Komanya, Stella Majaliwa na Ignas Mwinuka, umethibitisha mashtaka hayo pasipo shaka.
Jaji Sambo alisema ushahidi wa mashahidi 18, umethibitisha kuwa raia hao wa Kenya ndiyo walioshirikiana kwa pamoja, kumuua polisi huyo ambaye taifa bado lilikuwa likihitaji utumishi wake.
“Kulikuwa na hoja ya utetezi kuwa hawakutambuliwa kikamilifu lakini PC Naftali Ashery aliyekuwa lindo na marehemu aliwatambua vilivyo wauaji hao tena kwa ukaribu,” alisema. Alisema Mahakama imeridhika kuwa maungamo waliyoyatoa mbele ya walinzi wa amani ambao ni mahakimu waliyatoa kwa hiari bila kushurutishwa.
Mahakama imeukataa utetezi wa washtakiwa hao kuwa wakati wa mauaji hawakuwa nchini, akisema ushahidi wa vinasaba (DNA), umethibitisha walikuwapo nyumbani kwa mshtakiwa Kanje.
Jaji alisema kwa kuwa washtakiwa hao walikwenda kwa Kanje na yeye akawasaidia wasikamatwe na kuwatorosha, hilo ni kosa la kusaidia wahalifu baada ya kufanya mauaji.
Jaji Sambo alisema Kanje ndiye aliyeficha gari aina ya Toyota Land Cruiser mali ya Mahakama ya Kimataifa ya Rwanda (ICTR), lililotumika katika ujambazi huo na kwamba ushahidi wa wafanyakazi wawili wa mshtakiwa huyo, unathibitisha kuwa ndiye aliyetoa maelekezo kwa dereva wake ili akalitelekeze gari hilo eneo la Uwanja wa Ndege wa KIA.
Mahakama hiyo imeamuru kiasi cha fedha, Dola 8,145 za Marekani na Sh1,769,000 walizokutwa nazo raia hao wa Kenya, zikabidhiwe Benki ya NMB, Mwanga zilikoibwa.
Washitakiwa hao, Samweli Gitau Saitoti na mwenzake Michael Kimani walitiwa hatiani kwa kosa hilo na kufungwa kwenda jela miaka 30 kila mmoja huku Mtanzania mwengine, mshitakiwa namba 10, Elizabeth Msanze "Bella", mkazi wa kwangulelo mkoani Arusha, akihukumiwa kwenda Jela miaka 7.

Wasitakiwa hao wote kwa pamoja walikuwa wanakabiliwa na shtaka la mauaji ya kukusudia ya askari polisi katika shauri la namba 6 ya mwaka 2011, ambapo ilidaiwa kuwa wakiwa na wenzao wengine 9, walishiriki katika tukio la uporaji na mauaji yaliyotokea, Julai 11 mwaka 2007 katika Benki ya NMB tawi la Mwanga, wilayani Mwanga , mkoani Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad