TANAPA MEDIA AWARDS 2013 : WASHINDI WA TANAPA MEDIA AWARDS 2013 WAJICHUKULIA ZAWADI ZAO, RADIO 5 ARUSHA NA STAR TV ZANG'ARA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 May 2014

TANAPA MEDIA AWARDS 2013 : WASHINDI WA TANAPA MEDIA AWARDS 2013 WAJICHUKULIA ZAWADI ZAO, RADIO 5 ARUSHA NA STAR TV ZANG'ARA

Mshereheshaji Sauda Simba Kilumanga akiwakaribisha wageni katika ukumbi wa JB Belmont jijini Mwanza kwa ajili ya sherehe za utolewaji wa Tuzo kwa Wanahabari zinazoandaliwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa,Tanzania(TANAPA)Paschal Shelutete akifanya utamburisho wa wageni mbalimbali waliofika katika shughuli hiyo.
Baadhi ya wageni mbalimbali katika shughuli hiyo.
Meza kuu iliongozwa na Waziri wa Maliasili na Mazingira ,Lazaro Nyarandu.
Waziri Nyarandu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Ibrahim Mussa.
Mmoja kati ya wageni waalikwa alikuwa ni Mkurugenzi wa Umoja wa vilabu vya Waandishi wa Habari nchini ,Abubakar Karsan ambaye alipata nafasi ya kuzungumza machache.
Kiongozi wa Majaji waliofanya kazi ya kupitia kazi za Waaandishi walioshindanishwa na kisha kupatikana washindi Dk Ayoub Rioba akizungumza namna washindi walivyopatikana na baadae kuwatambulisha Majaji wenzake.
Majaji walioshiriki kufanya kazi ya kupitia kazi za washiriki .
Wageni mbalimbali wakifutilia shughuli hiyo.
Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu ,akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa,Allan Kijazi,Mkurugenzi wa Utalii na Masoko Ibrahimu Mussa pamoja na Meneja Ujirani Mwema Ahmed Mbugi tayari kwa zoezi la utolewaji wa TUZO HIZO.
Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoa mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni moja na laki tano kwa mshindi namba mbili wa uandaaji wa vipindi vya Radio,Humphrey Mgonja wa Radio SAUT fm.

Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akikabidhi mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni mbili pamoja na Ngao kwa mshindi namba moja wa uandaaji wa vipindi vya Radio,David Rwenyagira wa Radio 5 FM.

Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoa mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni moja kwa mshindi namba tatu kwa waandaji wa vipindi vya Televisheni ,Kakuru Msimu wa Star TV.

Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoa mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni moja kwa mshindi namba tatu upande wa Magazeti ,Salome Kitomary wa gazeti la Nipashe.
Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoa mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni moja na laki tano kwa mshindi namba mbili kwa waandaji wa vipindi vya Televisheni ,Raymond Nyamwihula wa Star TV.
Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoa mfano wa Hundi ya kiasi cha Sh Milioni mbili pamoja na Ngao kwa mshindi namba moja  kwa waandaji wa vipindi vya Televisheni ,Vedasto Msungu wa ITV.
Baadae David Rwenyagira alipata nafasi ya kutoa neno la shukrani kwa niaba ya washidi wa tuzo hizo.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la hifadhi za Taifa ,Tanzania ,Allan Kijazi akitoa neno na kisha kumkaribisha mgeni rasmi katika shughuli hiyo ,Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyarandu.
Mgeni rasmi katika sherehe za utolewaji wa Tuzo zijulikanazo kama TANAPA Media Award 2013,Waziri wa Maliasili na Utalii ,Lazaro Nyarandu akitoahotuba yake mara baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa tuzo.
Mwanamuziki Nguli wa muziki wa Bendi hapa nchini King kii a.k.a Mzee wa Kitambaa Cheupe na bendi yake alitoa burudani kwa washindi pamoja na wageni waalikwa.
Kila mmoja aliweka kitambaa Cheupe juu.
Baadae likafuatia neno la shukrani toka kwa Mkurugenzi wa Utalii na Masoko ,Ibrahimu Mussa.
Mgeni rasmi akapata picha ya pamoja na washindi.
Watu wa Star Tv ,Bernad James,Yvona Kamutu pia walikuwepo kutoa Pongezi kwa mwenzao Raymond Nyamwihula.
Picha na Dixon Busagaga.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad