KATIBU WA CCM ASEMA : ATAWABURUZA KWA RAIS VIONGOZI WA MKOA WA MANYARA WASIOTIMIZA WAJIBU WAO - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Friday, 30 May 2014

demo-image

KATIBU WA CCM ASEMA : ATAWABURUZA KWA RAIS VIONGOZI WA MKOA WA MANYARA WASIOTIMIZA WAJIBU WAO

01
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akilakiwa   kwa shangwe alipowasili kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ayamango katika Jimbo la Babati Vijijini, mkoani Manyara. Kinana yupo mkoani Manyara kwa ziara ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusukuma ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya CCM, kukagua maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.Tayari kafanya ziara hiyo katika mikoa ya Tabora na Singida.
02
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akilakiwa   kwa shangwe alipowasili kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ayamango katika Jimbo la Babati Vijijini, mkoani Manyara. 
03

IMG_1069
 Wananchi wa Kijiji cha Ayamango, Babati Vijijini wakiwa na bango la asili lenye maandishi yanayosisitiza umuhimu wa kuendelea na Muungano wa Serikali mbili badala ya tatu.
IMG_1083
 Wazee wa Kijiji cha Ayamango wakimvisha mgolole,Kinana ikiwa ni heshima ya kuwa mmoja wa wazee wa kijiji hicho.
IMG_1089
 Wanachama wa CCM wakila kiapo cha utii cha chama hicho wakati wa mkutano huo wa hadhara.
IMG_1097
 Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Ayamango, Babati Vijijini. ambapo alikerwa kwa kiasi kikubwa na jinsi wananchi wanavyoporwa maeneo yao na viongozi wa chama na Serikali ambapo aliahidi suala hilo kulitafutia ufumbuzi kwa kulipeleka katika vikao vya juu vya chama hicho.
IMG_1105
 Kinana akiwasikitishwa jinsi wananchi vijijini wanavyoporwa ardhi na kutumia mahakama kuchelewesha haki zao
.Kinana amesema kuwa viongozi wasiotimiza wajibu wao Mkoa wa Manyara atawaburuza kwa Rais.
IMG_1119
IMG_1118
 Vijana wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi za umoja wa vijana wa CCM kwenye mkutano huo
IMG_1096
 Wananchi wakiwa na bango linalosisitiza kendelea na mfumo wa Serikali mbili badala ya tatu
IMG_1042
Kikundi cha vijana kikitumbuiza wakati wa msafara wa Kinana ulipowasili katika Kijiji cha Ayamango.
PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *