MABOMU YALIVYORINDIMA : POLISI WATUMIA MABOMU KUWATAWANYA WAKULIMA WALIOFUNGA BARABARA ENEO LA MELELA MOROGORO - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Friday 7 February 2014

MABOMU YALIVYORINDIMA : POLISI WATUMIA MABOMU KUWATAWANYA WAKULIMA WALIOFUNGA BARABARA ENEO LA MELELA MOROGORO


Vijana wa Wakulima wakichoma matairi katikati ya barabara na kuzuia magari kutopita eneo hilo kwa muda wa masaa sita, jambo lililosababisha foleni kubwa ya magari na usumbufu kwa abiria, leo mchana. Askari wa kuzuia ghasi walilazimika kutumia Risasi za moto na mabomu ya machozi ili kuwatawanya watu hao na kuwafungulia njia abiria waliokuwa wamekwama mahala hapo kwa zaidi ya masaa sita.
Askari wakitoa tahadhari ya hatari kabla ya kuanza kuwatawanya vijana hao wa wakulima, ambapo walilazimika kuwatawanya wakulima wa eneo la Melela, Mvomero mkoani Morogoro waliokuwa wamefunga barabara ya Iringa - Morogoro wakimtaka Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera aende kusuluhisha mgogoro uliopo baina yao na wafugaji. 
Wakulima hao wanadai kuwa wenzao watano jana wamevamiwa na wafugaji wa kabila la Wamasai na kuwajeruhi vibaya kwa vitu vyenye ncha kali sehemu za siri na kupelekea kulazwa katika Hospitali ya Mkoa Morogoro.

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka alifika katika eneo hilo ambapo wananchi hao walikuwa wamechoma matairi na kusababisha msongamano mkubwa wa magari yaendayo Iringa na yale yaelekeayo Morogoro, lakini wakulima hao walikataa kumsikiliza wakimtaka mkuu wa mkoa.

Baada ya vurugu kuwa kubwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, aliwaaamuru vijana wake kuwatawanya wakulima hao ambao waligoma na kuanza kurusha mawe na askari hao wakajibu mapigo kwa kupiga mabomu ya machozi na kufanikiwa kuwatawanya.

Katika tukio hilo jumla ya wananchi takribani 20 wamekamatwa na polisi katika vurugu hizo.
Askari akiondoa baadhi ya miti na magogo yaliyokuwa yamewekwa katikati ya barabara hiyo.

No comments:

Post a Comment