UFUNGUZI WA KANISA LA OLASITI : BALOZI WA PAPA KUZINDUA KANISA LA MT. JOSEPH MFANYAKAZI LEO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Dec 2013

UFUNGUZI WA KANISA LA OLASITI : BALOZI WA PAPA KUZINDUA KANISA LA MT. JOSEPH MFANYAKAZI LEO

Mafundi wakikamilisha hatua za mwisho jana.
Makaburi ya watu watatu waliouawa na mabomu May 5,mwaka huu.
Maandalizi ya vya mwilini.
Mafundi wakijenga eneo lilipotua Bomu kama kumbukumbu ya kudumu iliyopoteza maisha ya watu na kujeruhi.
 
 Na Filbert Rweyemamu -Arusha
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini,Fransisco Padilla anatarajiwa kuzindua Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Olasiti leo ambalo lilikua lizinduliwe May 5 mwaka baada ya kutokea shambulio la bomu la kutupwa kwa mkono.
Mkuu wa mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo amewataka waumini na wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi  kanisani hapo kwani  ulinzi umeimarishwa kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa.
Alisema mbali ya Balozi wa Papa watakuwepo maaskofu wote kutoka baraza la maaskofu katoliki nchini(Tec)viongozi mbalimbali wa taasisi na serikali.
Kwa upande Mwenyekiti wa Parokia hiyo,Julius Mbaga alisema maandalizi ya uzinduzi yamekamilika na waumini wamejiandaa kiroho na kimwili katika siku hiyo muhimu.
“Tunatarajia wageni watu wasiopungua 3,000 na mambo matatu yatafanyika kwa wakati mmoja,Balozi Padilla atafungua kanisa letu na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha,Josephat Lebulu atatabaruku na kuweka wakfu nyumba za madri,”alisema Mbaga
May 5,mwaka huu wakati wa uzinduzi wa kanisa hilo lilifanyika shambulio la kigaidi lililosababisha vifo vya watu watatu na wengine kujeruhiwa vibaya na Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliahidi wahusika kusakwa popote walipo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad