WAFAHAMU MABALOZI WA KAMPENI YA GROW TOKA OXFAM,DINA MARIOS ,KIPANYA ,SHAMIM MWASHA, HALIMA MDEE... - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Wednesday, 3 July 2013

demo-image

WAFAHAMU MABALOZI WA KAMPENI YA GROW TOKA OXFAM,DINA MARIOS ,KIPANYA ,SHAMIM MWASHA, HALIMA MDEE...


g18
Ijumaaa ya tarehe 14 june Da. Dina Marios Mtangazaji wa kipindi Cha Leo Tena cha Clouds Fm na wenzake 6 walisimikwa kuwa Mabalozi wa Oxfam Tanzania katika  kampeni ya GROW.
Kusimikwa huko kuliambatana na tuzo maalum ya kutambulika kwa mchango wao katika kampeni hizo.
jacobstevenbalozigrowkampeni
Muigizaji maarufu wa Filamu za Ki bongo Bw. Jackob Steven JB "Eric Kiford".
khadijamwanambokabalozioxfamgrowkampeni
Mbunifu wa mitindo Tanzania Khadija Mwanamboka
masoudkipanyabalozigrowkampeniyaoxfam
CARTOONIST,MTANGAZAJI na Mtayarishaji wa vipindi vya TV Masoud Ally wa "Kipanya"
shamimmwashabalozigrowkampeniyaoxfamtz
Blogger maaarufu Shamimu Mwasha
Mabalozi wengine ni mbunge wa jimbo la Kawe Mh. Halima Mdee na mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Mh. Shyrose Bhanji.
g8 
Mkurugenzi wa OXFAM  Tanzania Justin Morgan
TAKWIMU zinaonyesha, tuko watu Bilioni Saba ulimwenguni hadi sasa.
TAKWIMU hizo hizo zinaonyesha, kati ya hao, takribani watu Billion moja hulala na njaa kila siku hiyo ikiwa ni tafsiri ya takribani mtu MMOJA kati ya watu SABA.
USHAHIDI upo kwamba chakula kinachozalishwa kinatutosha kula hadi kusaza.
USHAHIDI upo masokoni na sehemu za kuuza chakula jinsi ambavyo chakula hasa mboga mboga na matunda vinavyotupwa baada ya kuharibika.
USHAHIDI upo kwenye mashimo ya taka tunapotupa mabaki ya chakula.
USHAHIDI upo mashambani kwa wakulima wadogo wadogo wanaoacha mazao kuharibikia shambani kwa kukosa soko.USHAHIDI upo kwenye supermarkets chakula kinapotupwa kwa sababu kime-expire..
MAKADIRIO ni kuwa kufikia mwaka 2050 tutakuwa watu Bilioni Tisa ulimwenguni.
USHIRIKIANO ni msingi sasa kuhakikisha tunawezesha mfumo wa chakula kuwa wa HAKI na USAWA. Hii ni kuanzia shambani hadi jikoni.
images
 Balozi mwingine ni mwanamuziki maarufu wa Afrika Angelique Kidjo
2ace37a2fdee5a663e7d59af972fb5b4
Mchungaji Desmond Tutu
7260_633593126652976_1552241410_n
Asilimia 70 ya wakulima na wauzaji wa mazao ni wanawake.
 GROW inataka tuoteshe na kuimarisha uzalishaji na upatikanaji wa Chakula, uimarishaji wa haki na mustakabali wa wanawake wazalishaji wa Chakula na pia kulinda mandhari ya uoto na uhalisia wa sayari yetu.
944432_632579296754359_1985262058_n
GROW ni kampeni ya kimataifa inayoendeshwa na shirika la Oxfam. Kampeni hii inataka tuoteshe na kuimarisha uzalishaji na upatikanaji wa chakula, uimarishaji wa haki na mustakabali wa wanawake wazalishaji wa chakula na pia kulinda mandhari ya uoto na uhalisia wa sayari yetu.
Dunia inazalisha chakula cha kutosha lakini watu wapatao milioni moja wanalala bila kula kila siku. Mbaya zaidi, idadi kubwa ya hao ni wanawake wazalishaji na watoto.
Ni wakati muafaka sasa, kuungana na kutokomeza mfumo huu dhalimu wa chakula.
Namna tutakavyokuwa tunafanya kazi zetu za kibalozi mtafahamu kupitia vyombo mbali mbali vya habari.
Na mie kama balozi ntawahabarisha hapa na katika leo tena.
Picha kwa hisani ya Dina Marios Blog.

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *