MATUKIO MBALI MBALI KATIKA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH OLASITI JIJINI ARUSHA - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

6 May 2013

MATUKIO MBALI MBALI KATIKA MLIPUKO WA BOMU KATIKA KANISA LA MT. JOSEPH OLASITI JIJINI ARUSHA

DSCN2226 DSCN2228Ulinzi ukiimarishwa eneo ulipotokea mlipuko huo na kujeruhi makumi ya waumini.
DSCN2236
DSCN2267Mkuu wa Mkoa wa Arusha, magesa Mulongo akipata maelezo toka kwa padri wa kanisa la Mt Joseph Olasiti ambapo mlipuko huo umetokea..

Mlipuko unaodhaniwa kutokana na bomu la kurushwa kwa mkono umetokea katikati ya ibada katika kanisa katoliki la Mt Joseph lililopo Olasiti Jijini Arusha ambako kwa siku ya leo kulikuwa na ibada ya Kuzindua Parokia ya Mt Joseph Olasiti.
Mlipuko huo unaelezwa kutokea majira ya katikati ya saa nne na saa tano asubuhi wakati Askofu wa Kanisa hilo akiendelea na ibada. Ibada hiyo sambamba na uzinduzi husika imeahirishwa hadi wakati mwingine.
Balozi wa Papa na ujumbe wake walikuwa miongoni mwa wageni muhimu katika tukio hilo la uzinduzi. Balozi huyo Mhashamu Askofu Franscisco Padilla alikuwa Arusha toka alhamisi ya Mei 2, 2013 na alipatiwa ulinzi wa kutosha na Jeshi la Polisi.
Haijaweza kuthibitika hasa sababu za wahusika kurusha “bomu” lakini mmoja wa washukiwa tayari ametiwa nguvuni na Polisi.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa takribani watu watatu wamefariki na zaidi 66  kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa hospitali ya Mt Meru kwa matibabu.
Viongozi mbalimbali wa kijamii na kiserikali wameweza kufika eneo la tukio, miongoni mwao akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, Meya wa Manispaa ya Arusha, Gaudence Lyimo, na Mbunge wa Arusha Mjini Mh Gobless Lema.
Wengine ni Mbunge wa Arumeru Mashariki, mh. Joshua Nassari, Diwani Msofe wa Kata ya daraja Mbili (CHADEMA), diwani wa Kata ya Olasiti na viongozi wengine wa Jeshi la Polisi na usalama Mkoa na Wilaya.

Jengo la kanisa halijadhurika lakini taharuki miongoni mwa watumiaji wa jengo hilo wakiwemo waumini wa kaisa hilo ni kubwa.

Chanzo  cha  mlipuko  huo  inasemekana   kuwa  kuna  gari  ndogo  ilifika  kanisani  hapo  na  kusimama. Baadae  alishuka  mtu  aliyekuwa  amevalia  vazi  mithili  ya  kanzu  na  kurusha  kitu  kuelekea  kanisani  ambacho  ndicho  kilichosababisha  mlipuko  huo..
Lema hospitaliniMbunge wa Arusha mjini Godbless Lema akiwa na mbunge wa Arumeru Joshua Nassari wametoa damu kwa ajili ya majeruhi walioumia katika mlipuko huo.

Lema amewahimiza wakazi wa Arusha na vijana kujitolea kwa wingi kuchangia damu ili kuokoa maisha ya majeruhi.  Watu wengi wameitikia wito na  wanaendelea kujitolea kuchangia damu kama ishara ya kumuunga mkono mbunge wao.

DSCN2227Hali ya eneo mlipuko ulipotokea
DSCN2220Waumini na wananchi wengine wakiwa na shauku ya kujua kilichotokea
DSCN2228Ulinzi umeimarishwa
DSCN2252Viongozi wa Kanisa wakitoa taarifa ya kilichotokea kwa waandishi wa habari kabla ya Balozi wa Papa kuondolewa Kanisani hapo chini ya ulinzi mkali wa Polisi.
DSCN2246Wanasualama Mkoa wa Arusha, wakijadiliana jambo katika eneo la tukio
DSCN2282Meya wa Manispaa ya Arusha, Mh gaundence Lyimo akielekea eneo la tukio kwa miguu baada ya utaratibu wa kutumia magari kuwa mgumu kutokana na idadi kubwa ya watu na magari yaliyoziba njia.
DSCN2258Magesa Mulongo akiteta na RCO wa Mkoa wa Arusha
DSCN2273Mkuu wa Mkoa wa Arusha, magesa Mulongo akijiandaa kuzungumza na wananchi kanisani hapo na kuahidi kuwa Serikali itahakikisha watu wote waliohusika na jaribio hilo ovu, pamoja na mtandao wao wanakamatwa. Alidai pia vikosi vya Jeshi maalumu kwa kuchunguza milipuko vitafika eneo hilo ili kufanya uchunguzi. Taarifa za eneo la tukio zinaeleza kuwa tayari kuna mshukiwa mmoja ameshatiwa mbaroni na yuko mikononi mwa Jeshi la Polisi kwa mahojiano na uchunguzi zaidi.
DSCN2236Eneo lenye utepe ndipo kitu hicho kinachodhaniwa kuwa bomu kilipoangukia. Pichani unaweza kuona wigi za kichwani na viatu vya waumini vikiwa vimesambaa baada ya wenyewe kuviacha, miongoni mwao wakiwa ni majeruhi.
DSCN2251Balozi wa Papa akisindikizwa na ulinzi mkalai kutoka kanisani hapo
DSCN2267Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo akizungumza na mmoja wa mapadri wa Kanisa hilo kupewa maelezo ya kuhusu kilichotokea kanisani hapo.
DSCN2276
DSCN2255
DSCN2281
Picha kwa hisani ya Arusha 255 Blog

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633