JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
UZIMAJI WA MITAMBO
YA KURUSHA MATANGAZO YA TELEVISHENI YA MFUMO WA UTANGAZAJI WA ANALOJIA ARUSHA
31 MARCH 2013
Uzimaji
wa mitambo ya utangazaji wa Televisheni ya mfumo wa analojia ulianza
kutekelezwa tarehe 31/12/2012 saa sita kamili usiku katika jiji la Dar es
Salaam kwa makubaliano ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Uzimaji
wa mitambo ya analojia umefinyika pia katika niji ya Dododma na Tanga tarehe
31/01/2013 na Mwanza tarehe 31/02/2013.
Kulingana
na ratiba iliyotolewa na serikali mnamo mwezi desemba 2012 ,miji inayofuatia
kuzima mitambo ya analojia ni Moshi na Hapa Arusha.
Maandalizi
ya kuzima mitambo ya nalojia ya utangazaji wa televisheni kwa Arusha ,
yamekamilika kwa kushiriikiana na wadau wa sekta ya utangazaji hapa Arusha.
Mitambo itazimwa saa sita kamili usiku.
Elimu
kwa umma kupitia mbinu mbalimbali kuhusu mchakato wa kuhamia katika teknolojia
ya mfumo wa utangazaji wa dijitali imekuwa ikitolewa kwa kiwango cha
kuridhisha. Matangazo ya dijitali yanawafikia watu asilimia zaidi ya 20% kati a
watu asilimia 24% wanaopata matangazo ya televisheni ya analojia .
Serikali
ilifikiria kwa kina zoezi zima la kuzima mitambo ya televisheni ya teknolojia
ya analojia kwa makini sana. Ili kufanikisha zoezi hili bila kuwa na usumbufu
mkubwa ,serikali iliweka ratiba ya uzimaji kama ifuatavyo:
- Dar es Salaam – 31 Desemba
2012; Tayari mitambo ilishazimwa
- Dodoma & Tanga – 31 Januari
,2013 :Tayari mitambo imeshazimwa
- Mwanza – 28 Februari ,2013 ;
tayari mitambo ilishazimwa
- Arusha & Moshi – 31 Machi
,2013; mitambo itazimwa
- Mbeya – 30 Aprili ,2013;
mitambo itazimwa
Kama
ilivyoolezwa tangu awali,utaratibu wa kuzima mitambo ya analojia utakuwa kwa
maeneo yenye matangazo ya digitali tu. Maeneo ambayo hayana miundombinu ya
dijitali hayatazimwa kwa sas hadi yapate dijitali.
Mabadiliko
haya hayahusu matangazo kwa njia ya utangazaji wa Sarelaiti , waya (cable) na Redio. Tunawataka wananchi wa Mkoa wa
Arusha wasitupe TV zao za analojia bali wanunue ving’amuzi ili kupata matangazo
ya dijitali.
Mamlaka
ya Mawasiliano imeagiza watoa huduma za kusambaza ving’amuzi walioko Arusha
kuhakikisha kuwa kunakuwa na Ving’amuzi vya kutosha. Tumefanya ukaguzi katika
mji wa Arusha na tumehakikisha vuko ving’amuzi vya kutosha na tumehakikishiwa
kuwa vingine viko njiani kuja mjini Arusha kati ya leo au kusho ambako zaidi ya
ving’amuzi zaidi ya 5000 vitakuwa madukani.
Serikali
inatarajia kupata ushiriakiano wa karibu kutoka kwa wadau wa sekta ya
utangazaji na wananchi kwa ujumla katika kipindi cha uzimaji wa mitambo ya
utangazaji wa televisheni ili kufanikisha zoezi la uzimaji wa mitambo ya
utangazaji ya teknolojia ya analojia.
Imetolewa
na:
Mkurugenzi
Mkuu
Mamlaka
ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Machi
27,2013 – ARUSHA.
|
No comments:
Post a Comment