LULU ATOKWA NA MACHOZI KWA KUWA NJE YA MAHABUSU KWA DHAMANA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Jan 2013

LULU ATOKWA NA MACHOZI KWA KUWA NJE YA MAHABUSU KWA DHAMANA

Lulu akiwa amezungukwa na baadhi ya waandishi wa habari waliotala kufanya nae mahojiano mfupi baada ya kupata dhamana.
Lulu akiangua kilio baada ya kushindwa kuongea na waandishi wa habari waliokusanyika mahakamani hapo.

AKIWA amesota mahabusu kwa takribani siku 274 au  miezi tisa hatimae Msanii machachari wa filamu nchini Elizabeth Michael “Lulu” anayekabiliwa na mashitaka ya mauaji bila kukusudia ya  Steven Kanumba ametoka mahabusu kwa dhamana. 

Dhamana hiyo ilitolewa jana katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaama baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa jna Jaji Zainab Mruke.

Alitimiza masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaofanyakazi serikalini, ambao wamesaini hati ya Sh milioni 20 kila mmoja, amewasilisha mahakamani hati zake za kusafiria, anatakiwa kuripoti mahakamani tarehe mosi ya kila mwezi na kutosafiri nje ya Dar es salaam bila ruhusa ya msajili wa mahakama.

Lulu alifikishwa mahakamani hapo jana saa 7:50 mchana akiwa kwenye gari la polisi lenye namba za usajili STK 2823 na kufikishwa mbele ya Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam Francis Kabwe kwajili ya kukamilisha taratibu za dhamana. 

Mtuimishi wa Wizara ya Ardhi Florian Mutafungwa pamoja na Dkt Verus Kataruga kutoka Wizara ya Afya ambapo saa 10:00 alitoka chini ya ulinzi baada ya kukamilisha masharti ya dhamana. 

Lulu aliwasilisha maombi ya dhamana chini ya hati ya dharura akiomba yasikilizwe na kuamriwa haraka kwa kuwa amekaa rumande kwa muda mrefu na kosa lake lina dhamana.

Akitoa uamuzi wa ombi la dhamana ya Lulu lililowasilishwa, Jaji Mruke alisema Mahakama imekubali ombi hilo kwa kuwa, shitaka linalomkabili linadhaminika na dhamana ni haki yake ya msingi .

Akizungumza baada ya kupewa dhamana, Lulu aliwashukuru watu wote walikuwa wanamsaidia katika kipindi  chote tangu alipokamatwa hadi anapata  dhamana na kuomba waendelee kumuombea.

“Nawashukuru watu wote lakini naomba muendelee kuniombea kwa kuwa huu ni mwanzo tu kesi hii bado ndio kwanza inaanza” alisema Lulu huku akitokwa na machozi. 

Aliondoka  na gari gari lenye namba za usajili T 480 CFX Kwa upande wake Wakili wa Lulu, Peter Kibatala alisema, dhamana ni mkataba kati ya mshitakiwa na mahakama na kuna taratibu za kufuata ndio maaana walichelea lakini anashukuru msajili kwa kusubiri hata baada ya muda wa kazi kuisha ili Lulu apate halki yake ya msingi.

Lulu alitakiwa kupewa dhamana juzi hata hivyo alirudishwa rumande kwa kuwa alichelewa kuwasilisha mahakamani hati yake ya kusafkiria hadi msajili alipoondoka baada ya saa za kazi kuisha.

Kesi hiyo ilifunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu huku Lulu akikabiliwa na mmashitaka ya kumuua Kanumba kwa kukusudia hata hivyo baada ya upelelezi kukamilika, Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) alimbadilishia mashitaka na kuwa kuua bila kukusudia shitaka ambalo lina dhamana.

Baadaye kesi hiyo ilihamishiwa katika Mahakama Kuu na kusajiliwa kama shauri la kuua bila kukusudia lenye namba 125 ya mwaka jana, na kupangwa kusikilizwa mbele ya Jaji Mruke. Hata hivyo kesi hiyo bado haijpangiwa tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Lulu anadaiwa Aprili 7 mwaka jana katika eneo la Sinza Vatican, alimuua msanii Kanumba bila kukusudia.

Baada ya kutoka mahakamani Lulu alipokewa na Mama yake, na wasanii wenzake Dkt Cheni, Abdukarim Kenyata “Mc Kenyata na Muna pamoja na ndugu zake wengine. Na Father Kidevu Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad