Timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam leo imefanikiwa kuitoa timu ya St. George ya Ethiopia, baada ya kuiondosha katika mashindano ya Kombe la Kagame Castle Cup kwa penati 5-4 kwenye mchezo wa nusu fainali ,uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Tanzania leo.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa ni wa vuta nikuvute kwa kila upande hakuna timu iliyofanikiwa kuliona lango la mwenzake, hata hivyo ziliongezwa dakika 30 baada ya kipindi cha kawaida cha dakiki 90 kumalizika kwa sare ya 0-0. Kwa maana hiyo Yanga itakutana na watani wao wa jadi timu ya Simba ya Tanzania pia ambayo ilifanikiwa kutinga fainali jana, baada ya kuikung'uta timu ya El Mereck ya Sudan kwa penati 6-5 pia.
Mchezo wa fainali unatarajiwa kuwa mgumu sana hapo jumapili kutokana na timu zote mbili kufahamiana vyema kimchezo, lakini akihojiwa na mtangazaji wa Supersport Thomas Mlambo kocha wa Yanga Sam Timbe, Amesema "Simba imejiandaa vizuri kwani imecheza michezo kadhaa mikubwa na timu zilizoko kwenye viwango vya juu, kama vile TP Mazembe Motema Pembe na zingine ukilinganisha na timu yake ya Yanga". Hata hivyo ameongeza kuwa "muda uliopo unatosha ataangalia mapungufu na kuyarekebisha kwa ajili ya mchezo wa fainali, ambao anaamini utakuwa mzuri na wenye ushindani mkubwa" Amemaliza Sam Timbe.
STANDARD CHARTERED YAONGOZA TUKIO LA UPANDAJI MITI BAGAMOYO.
-
Kama sehemu ya dhamira yake ya kukuza uendelevu wa mazingira na uhifadhi wa
mazingira, Standard Chartered Tanzania imeongoza shughuli ya upandaji miti
ka...
39 minutes ago
No comments:
Post a Comment