VODACOM TANZANIA YAFANYA HAFLA YA KUWABURUDISHA WABUNGE USIKU HUU KATIKA VIWANJA VYA BUNGE MJINI DODOMA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Jul 2011

VODACOM TANZANIA YAFANYA HAFLA YA KUWABURUDISHA WABUNGE USIKU HUU KATIKA VIWANJA VYA BUNGE MJINI DODOMA


Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda akizungumza na wageni waalikwa mbalimbali katika hafla ya kuburudisha ya wabunge na kutambulisha nembo nyekundu na mpya ya kampuniya Vdacom Tanzania kwenye hafla hiyo iliyofanyika usiku huu katika viwanja vya bunge mjini Dodoma, huku mgeni rasmi akiwa Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Mizengo Pinda, FULLSHANGWEBLOG imetia timu mjengoni kwa ajili ya kukumuvuzishia matukio usiku huu endelea kupata uhondo kutoka viwanja vya bunge.
Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Anne Makinda akimkaribisha Waziri Mkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo usiku huu.
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akisakata Rhumba na Spika wa bunge Mh Anne Makinda katika hafla ya kuburudisha wabunge iliyoandal;iwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania iliyofanyika katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mh. Freeman Mbowe akicheza muziki na mmoja wa wabunge bwa bunge la Jamhuri yaq muungano wa Tanzania katika hafla iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania.
Wadau wa Fullshangwe na walikuwepo katika hafla hiyo kulia ni Dailly na Jerry wakipozi kwa picha.
Waheshimiwa wabunge wakisakata rhumba katika hafla hiyo.
Diamond akiimba katika hafla hyo usiku huu.
Aliyewahi kuwa mshiriki wa Tusker Project Fame ambaye pia ni mwimbaji wa bendi ya B. Band Annet Kashaba akiimba katika hafla hiyo.
Diamond na Kundi lake la wacheza shoo waking'arisha hafla hiyo
Mbunge wa Tabora mjini Mh. Aden Rage akicheza na Naibu waziri wa Jinsia wanawake na watoto Mh. Ummy Mwalimu.
Waziri Mkuu wa Mh. Mizengo Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Vodacom Tanzania Dietlof Mare, wakati alipokuwa akiwasili katika hafla ya kuwaburudisha wabunge na kuitambulisha rasmi nembo nyekundu ya kampuni ya Vodacom,
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Anne Makinda kulia, na Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare mara baada ya kumpokea Mgeni Waziri mkuu.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda wa pili kushoto akiwasili katika hafla iliyoandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, kwa ajili ya kuburudisha wabunge jioni hii katika viwanja vya bunge. Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare akisalimiana na Kiongozi wa upinzani bungeni Mh. Freeman Mbowe katika sherehe hiyo.
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Dietlof Mare kulia akizunguza jambo na Spika wa bunge Mh Anne Makinda, katikati ni Mwamvita Makamba Afisa mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania.
Spika wa Bunge Mama Anne Makinda akifurahia jambo na Waziri ofisi ya Waziri mkuu sera uratibu na bunge William Lukuvi, katikati ni Mh. Simbachawene.
Wanamuziki wa muziki wa taarab Shakira kushoto na Patricia Hillary wakiimba katika hafla hiyo. Mwanamuziki Banana Zoro akifanya vitu vyake jukwaani katika hafla ya kuwaburudisha wabunge, iliyoandaliwa na kampuni simu za mkononi ya Vodacom Tanzania inayofanyika usiku huu katika viwanja vya Bunge.
Wabunge mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.
Waheshimiwa wabunge wakimkaribisha Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Banana Zorro akiimba katika hafla hiyo inayofanyika katika viwanja vya bunge mjini Dodoma usiku huu. 
 
Picha na matukio: Fullshangwe Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad