Mbio za kilomita 5 za maadhimisho ya siku ya vyombo habari Duniani zafanyika leo jijini Arusha, katika viwanja vya Ghymkana/ Mgambo.
Mbio hizo zilianzia kwenye uwanja wa Ghymkana /Mgambo na kumalizikia hapo hapo Ghymkhana; ambapo zilihudhuriwa na wanahabari mbalimbali , wadau wa habari na wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa.
Maadhimisho ya Vyombo vya habari duniani yanafanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 27 hadi 30 Aprili 2025, ambapo siku ya kwanza yameanza na mbio za kilomita 5 na kesho kutafanyika mikutano mbalimbali katika hoteli ya Gran Melia.
Maadhimisho hayo yanaratibiwa na JamiiAfrica au zamani Jamii Forums, Serikali , shirika la Kimataifa la Elimu , Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na wadau wengine wa Habari nchini na Kimataifa.
No comments:
Post a Comment