Matukio : Ziara ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoani Njombe. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


3 Mar 2018

Matukio : Ziara ya Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoani Njombe.




Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka alipomtembelea ofisini kwake kupata taarifa ya Viwanda na uwekezaji katika mkoa huo, leo tarehe 1 Machi, 2018.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri walipofika ofisi za SIDO Mkoa wa Njombe kuona utendaji wake.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akikagua eneo litakalojengwa majengo makubwa kwa ajili ya wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo, Mkoani Njombe leo tarehe 1 Machi, 2018.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage, akimsikiliza meneja wa Wakala wa Vipimo Mkoa wa Njombe kuhusu utaratibu wanaotumia katika kupima mizigo ya wakulima na wafanyabiashara mkoani Njombe.

Muonekano wa Kiwanda cha kuchakata Chai cha Unilever kilichopo mkoani Njombe ambacho kipo katika hatua za mwisho kukamilika kwa ujenzi wake.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akikagua uenzi wa kiwanda cha Chai cha Unilever, Mkoani Njombe leo tarehe 1 Machi, 2018.

Wadau na wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe waliokusanyika kumsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Hayupo pichani) na baadae kuuliza maswali kutokana na changamoto wanazokutana nazo na kupatiwa majibu.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza wakati wa mkutano na wafanyabiashara kujadili changamoto zianazowakabili wafanyabiashara katika mkoa wa Njombe Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bibi. Ruth Blasio Msafiri.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad