Utalii : Wazalendo 47 kutoka JWTZ na kundi la Wanahabari Walivyotumia Siku 5 Kupanda kilele cha Uhuru kwa ajili ya Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Dec 2017

Utalii : Wazalendo 47 kutoka JWTZ na kundi la Wanahabari Walivyotumia Siku 5 Kupanda kilele cha Uhuru kwa ajili ya Sherehe za Miaka 56 ya Uhuru.



Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) Betrita Loibok akizungumza katika hafla fupi ya kuagwa kwa wazelendo 47 waliopanda mlima Kilimanjaro.

Baadhi ya Washiriki katika changamoto ya kupanda Kilimanjaro kwa ajili ya kutangaza Utalii wa Ndani na utunzaji wa Mazingira.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akizungumza katika hafla ya kuwaaga washiriki wa changamoto ya upandaji wa mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kutangaza Utalii wa ndani na Utunzaji wa Mazingira.

Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Utalii Tanzania ,Balozi Charles Sanga (kulia) alikua ni miongoni mwa Wazalendo walioshiriki changamoto ya kupanda Mlima Kilimajaro.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu ,Jenerali George Waitara anayeshiriki zoezi la kupanda Mlima Kilimanjaro kwa mara ya 10 sasa akazungumza na washiriki wa zoezi hilo kabla ya kuianza safari.


Mkuu wa wilaya ya Rombo ,Agness Hokororo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuwaaga Wazalendo 47 kupanda mlima Kilimanjaro.
Mkuu wa Wilaya ya Rombo ,Agnes Hokororo akimkabidhi Bendera ya taifa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu,Jenerali George Waitara kabla ya kuanza kwa safari hiyo.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu,Jenerali George Waitara akikabidhi Bendera kwa Mkuu wa kamandi ya Brigedi ya Magharibi,Brigedia Jenerali Mkumbo aliyekuwa mkuu wa Msafara wa Wazalendo 47 waloshiriki kupanda Mlima Kilimanjaro.
Wazalendo 47 walioshiriki changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Rombo .Agness Hokororo.
Safari katika siku ya kwanza ya kuelekea kilele cha Uhuru ikaanza ,Mkuu wa Majeshi Mstaafu,Jenerali ,Georg Waitara akiongoza.
Kundi la Wanahabri lilikua na kazi ya kuchukua taswira za safari nzima ya kulekea kileleni.
Uzalendo wa kuifikisha Bendera ya Taifa katika kilele cha Uhuru ndio uliongeza morali kwa washiriki ya kuendelea na safari .


Wazalendo walipata mapumziko katika eneo la Nusu njia lijulikanalo kama Kisambioni na baadae kuendelea na safari.

Licha ya kuwepo kwa mvua ,bado safari ya Wazalendo 47 iliendelea.

Wengine walipatiwa msaada pindi walipohitaji ili mradi safari iwe rahisi.
Safari ya Wazalendo haikuwacha nyuma ,Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro ,Betrita Loibook na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete .walitembea licha ya kunyeshwa na mvua.

Wenye kiu walipata maji na baadae kuendelea na sfari.
Hatimae safari katika siku ya kwanza kwa Wazalendo 47 kuelekea kilele cha Uhuru ikakamilika mara baada ya kuwasili kituo cha mapumziko cha Mandara.Imeandaliwa na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,aliyekuwa katika safari hiyo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad