Uchumi : Sekta ya Viwanda Inahitaji Wahandisi wengi - Lema - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Oct 2017

Uchumi : Sekta ya Viwanda Inahitaji Wahandisi wengi - Lema



Mwenyekiti wa ALAT Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam wa pili kulia akipokea mifuko ya saruji 500 kutoka kwa Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Saruji ya Simba Cement Benedict Lema katikati ni Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Mkoa wa Tanga, Radhiya Msuya ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano ya Nje wa Simba Cement, Noor Mtanga




Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Saruji ya Simba Cement Benedict Lema wa pili kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 500 Mwenyekiti wa ALAT Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam wa pili kutoka kulia kwa ajili ya ujenzi miundombinu katika sekta ya elimu katikati ni Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Mkoa wa Tanga, Radhiya Msuya ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano ya Nje wa Simba Cement, Noor Mtanga

Sehemu ya Saruji iliyokabidhiwa

Meneja Uhusiano na Mawasiliano ya Nje wa Simba Cement, Noor Mtanga kulia akifafanua jambo kabla makabidhiano hayo leo kushoto ni Mwenyekiti wa ALAT Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Mkoa wa Tanga, Radhiya Msuya na Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Simba Cement,Benedict Lema wakimsikiliza meneja huyo wa Uhusiano na Mawasiliano ya Nje



Mwenyekiti wa ALAT Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam katikati akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhiwa Saruji hiyo

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Mkoa wa Tanga, Radhiya Msuya akizungumza na waandishi wa habari kuishukuru kampuni ya Simba Cement mara baada ya kushuhudia makabidhiano hayo kulia ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano ya Nje wa Simba Cement, Noor Mtanga kushoto ni




Mwenyekiti wa ALAT Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam,Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Simba Cement Benedict Lema anayefuatia kushoto ni Afisa Mawasiliano wa Simba Cement,Helleni Maleko

NA MWANDISHI WETU, TANGA.




IMEELEZWA kuwa sekta ya viwanda inahitaji wahandisi ambao watashiriki katika shughuli mbalimbali baada ya wale waliopo hivi sasa kustaafu kwa kuwekewa mazingira mazuri wanaochipukia katika uimarishaji wa miundombinu shuleni.

Hayo yalisemwa na Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Saruji cha Tanga (Tanga Cement),Benedict Lema wakati akikabidhi mifuko 500 ya Saruji kwa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Shinyanga Gulam Hafeez Mukadam kwa ajili ya shule zao katika kuboresha maendeleo na ujenzi wa vyoo vya wanafunzi na maeneo mengine ya elimu na afya.

Mifuko hiyo ina zaidi ya thamani ya milioni 6 iliyotolewa Halmashauri ya Shinyanga kwa ajili ya kuweza kukabiliana na uhaba wa miundombinnu ya shule ikiwemo vyoo.
Lema alisema ili kuweza kusaidia harakati za kuelekea Tanzania ya Viwanda ndio sababu kubwa wamekuwa wakitoa misaada mbalimbali kuwezesha kupunguza baadhi ya changamoto zilizopo ili kuhakikisha zinakwisha.




Aidha alisema wanafunzi wanapaswa kuongeza bidii ili kuweza kufanikiwa katika masomo yao jambo ambalo litawezesha kupatikana kwa wahandisi wengi ambao watasaidia sekta ya viwanda.




Awali akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Rasilimali watu na Utawala Mkoa wa Tanga, Radhiya Msuya aliishukuru kampuni ya Tanga Cement kwa mchango wao mkubwa wanaoutoa katika kusaidia sekta ya elimu ya vijana wetu ambao watakuwa wataalamu kwenye maeneo mbalimbali.




Alisema mchango wao huyo ni mkubwa kwa sababu unasaidia katika harakati za kuelekea Tanzania ya Viwanda kwa kuona mbali kwa kuwekeza kwenye sekta ya elimu ambayo ndio nguzo muhimu kufikia malengo hayo.




Naye kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT ) Taifa ambaye pia ni Mshtahiki Meya wa Shinyanga, Gulam Hafeez Mukadam aliishukuru kampuni hiyo kwa kuthamini harakati za kuinua elimu hapa nchini kwa kusaidia mifuko hiyo ya saruji ambayo itakuwa ni chachu kubwa kufikia malengo yao kielimu.




Alisema anawashukuru sana kwa kuunga mkono agizo la Rais kuelekeza nguvu kwenye sekta ya elimu katika kutatua changamoto za madawati na vyoo ili kusaidia harakati za elimu ambazo zinafaida.




Hata hivyo alisema wataendelea kuwahimiza vijana kuhakikisha wanasoma kwa bidii ili kuweza kupatikana wahandisi wengi ambao watakuwa ni chachu kubwa baada ya waliopo kustaafu.


Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad