Uchumi :Injinia Stella Manyanya afanya ziara yake ya kwanza ya kikazi akiwa Wizara ya Viwanda - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


14 Oct 2017

Uchumi :Injinia Stella Manyanya afanya ziara yake ya kwanza ya kikazi akiwa Wizara ya Viwanda





Naibu Waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stella Manyanya afanya ziara yake ya kwanza ya kikazi akiwa Wizara ya Viwanda kwa kutembelea kongano la ngozi na bidhaa za ngozi katika eneo la zuzu Mkoani Dodoma.


Aidha Mhe. Waziri amewaagiza watendaji wa wizara kufanya juhudi za haraka za uendelezwaji wa eneo hilo kwa hakuna sababu ya kuchelewa ambapo mhe. Naibu waziri ametoa muda wa miaka miwili hilo eneo liwe limeanza kuwekewa miundombinu na huduma nyingine.


Pia mhe. Waziri ametembelea eneo la SIDO lililotengwa kwa ajili ya kongano la alizeti ambapo pia amewaagiza watendaji kufanya juhudi za haraka kuharakisha mchakato wa uendelezwaji wa eneo hilo, Mhe. Naibu waziri alihitimisha ziara yake kwa kutembelea ofisi za SIDO na kutembelea ajasiliamali walioko chini ya SIDO na kujionea shughuli za ujasiriamali zinazofanywa katika eneo hilo.


Mhe. Naibu waziri ataendelea na ziara ya kutembelea taasisi zilizo chini ya wizara kuanzia wiki ijayo na kujionea utendaji wa kila taasisi.

Darasa maalumu la mafunzo ya uzalishaji na utengezaji wa bidhaa za ngozi lililopo Kizota, mkoani Dodoma.

Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akishuhudia bidhaa mbalimbali zinazotengezwa na wanafunzi wanaojifunza utengezaji wa bidhaa za ngozi pembeni ni ndugu. Stephano Ndunguru, meneja wa mafunzo SIDO, Dodoma.

baadhi ya bidhaa za ngozi zinazotengezwa na wanafunji wanaojifunza utengezaji wa bidhaa za ngozi.

Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akizungumza na watendaji wa SIDO, Dodoma.


Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akiangalia bidhaa zinazotengezwa na wajasiriamali wa SIDO.

baadhi ya bidhaa za wajasiriamali wa SIDO, Dodoma.

Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akichomelea alipowatembelea wajasiriamali wa vyuma SIDO, Dodoma.

Naibu waziri, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Injinia Stellah Manyanya akikagua eneo maalumu kwa ajili ya kongano la ngozi, Zuzu mkoani Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad