Siasa : Wagombea kuweni Makini kwenye nafasi zenu - Dk. Dallo - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Aug 2017

Siasa : Wagombea kuweni Makini kwenye nafasi zenu - Dk. Dallo






Na Woinde Shizza,Arusha

Wagombea wa nafasi mbalimbali za ungozi ndani ya chama cha mapinduzi wilaya wa Arusha wametakiwa kufuata kanuni na sheria za zilizowekwa na chama hicho.

Hayo yamebainishwa na katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Arusha Dr, Ramathani Dallo wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na tuhuma za kuwepo na baadhi ya wagombea kuja kwenye usahili na watu wanaodaiwa sio wagombea bali ni waganga wa kienyeji

Alisema kuwa ni muhimu sana wagombea wakifuata kanuni taratibu na sheria zilizowekwa katika uchaguzi kwa mujibu wa kanuni ya muongozo wa uchaguzi ya mwaka 2010


Alisema kuwa yeye binafsi ajawaoana watu hao wanaodaiwa ni waganga wa kienyeji na usahili ulienda vizuri na k atika kipindi hichi uchaguzi unaendelea vyema ,huku akibainisha kuwa iwapo kutakuwa na mgombea yeyote ambae atakwenda kinyume na sheria ya uchaguzi atamuaonea huruma bali atuakali zidi yake itachukuliwa .

“nasema kwakweli ili swala na mgombea wa UWT kuja na mganga wa kienyeji kwenye usaili sijaliona ila ukweli napenda kuchukua nafasi hiii kuwasihi iwapo tutamkamata mgombea yeyote Yule anaekwenda kinyume na sheria tutamchukulia hatua kali za kisheria ikiwemo kuinta kikao kama jambo ni gumu sana pia itatulazimu tumkate jina lake na asiwepo kwenye kinyanganyiro chochote”alisema Dk. Dallo


Alizitaja baadhi yakanuni kuwa ni pamoja na kutofanya kampeni ,kukusanya watu kufanya mikutano isioyo rasmi kichama pamoja na nyingi

Aidha akiongelea baadhi za uchaguzi zilizopita alisema kwa upande wa uchaguzi wa kata ,mitaaa umemalizika vizuri sasa ivi ndio wanaendelea na maeneo mengine yaliyobaki


Awali baadhi ya wagombea ambao hawakutaka majina yao yaandikwe walisema kuwa kuna mmoja wa mgombea mwenza sik u ya usahili alikuja akiwa na mganga wa kienyeji kitu ambacho ni kinyume na sheria ya uchaguzi

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad