Nishati /Zanzibar : Shirika la Umeme Lapongezwa - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Tuesday, 8 August 2017

demo-image

Nishati /Zanzibar : Shirika la Umeme Lapongezwa



DSC_0499

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akitowa shukrani zake kwa Uongozi wa Shirika la Umeme Zanzibar kwa ushirikiano wao kuwezesha kupa umeme kwa wakati na katika kijiji cha Tunguu Uwandani Wilaya ya Kati Unguja, wakiwa katika sehemu iliowekwa Transfoma kwa ajili ya kupokea umeme katika kijiji hicho na kutowa huduma hiyo kwa wananchi zaidi ya mia moja kupata huduma hiyo.

DSC_0480

Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO Hassan Ali akitowa maelezo wakati wa hafla hiyo ya kupokea shukrani zilizotoka kwa Wananchi wa Jimbo hilo na Mwakilishi wao kwa msaada wao wa usambazaji wa umeme kwa wakati na kupata fursa ya kupata hudumi hiyo.

DSC_0457

Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Kijiji cha Tunguu Uwandani akitowa shukrani za wananchi wa kijiji hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika eneo lililowekwa transfoma ya kusabaza umeme katika eneo hilo na kutowa huduma kwa wananchi zaidi ya mia moja.

DSC_0464


Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kutowa shukarani kwa Shirika la Umeme Zanzibar kwa msaada wao kukamilisha zoezi hilo la usambazaji wa umeme katika Kijiji cha Tunguu Uwandani Wilaya ya Kati Unguja.hafka hiyo imefanyika katika kijiji hicho tunguu.

DSC_0471


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Mazingira Ally Halil Milza akizungumza wakati wa hafla hiyo na kuwataka wananchi wa kijiji hicho kuitumza miundo mbinu hiyo na kuahidi kusambaza umeme kwa wananchi wa vijiji jirani kwa kuongeza nguzo 16 zilizobakia ili kuweza kupatikana kwa huduma hiyo kwa wananchi hao.

DSC_0476


Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Tunguu Uwandani wakiwa katika eneo la hafla hiyo wakisikiliza nasaha zilizokuwa zikitolewa na wahusika.

DSC_0478


Sheha wa Shehia ya Tunguu Uwangani akisoma dua baada ya hafla hiyo kumalizika ya kutowa shukrani

DSC_0483


Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Mazingira Ally Halil Mirza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu na Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kijiji hicho baada ya kumalizika kwa hafla hiyo.

DSC_0503


Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe, Simai Mohammed Said akizungumza na wananchi wa Jimbo lake baada ya kumalizika kwa hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *