Nishati /Zanzibar : Shirika la Umeme Lapongezwa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


8 Aug 2017

Nishati /Zanzibar : Shirika la Umeme Lapongezwa





Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akitowa shukrani zake kwa Uongozi wa Shirika la Umeme Zanzibar kwa ushirikiano wao kuwezesha kupa umeme kwa wakati na katika kijiji cha Tunguu Uwandani Wilaya ya Kati Unguja, wakiwa katika sehemu iliowekwa Transfoma kwa ajili ya kupokea umeme katika kijiji hicho na kutowa huduma hiyo kwa wananchi zaidi ya mia moja kupata huduma hiyo.



Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO Hassan Ali akitowa maelezo wakati wa hafla hiyo ya kupokea shukrani zilizotoka kwa Wananchi wa Jimbo hilo na Mwakilishi wao kwa msaada wao wa usambazaji wa umeme kwa wakati na kupata fursa ya kupata hudumi hiyo.



Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Kijiji cha Tunguu Uwandani akitowa shukrani za wananchi wa kijiji hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika eneo lililowekwa transfoma ya kusabaza umeme katika eneo hilo na kutowa huduma kwa wananchi zaidi ya mia moja.




Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kutowa shukarani kwa Shirika la Umeme Zanzibar kwa msaada wao kukamilisha zoezi hilo la usambazaji wa umeme katika Kijiji cha Tunguu Uwandani Wilaya ya Kati Unguja.hafka hiyo imefanyika katika kijiji hicho tunguu.




Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Mazingira Ally Halil Milza akizungumza wakati wa hafla hiyo na kuwataka wananchi wa kijiji hicho kuitumza miundo mbinu hiyo na kuahidi kusambaza umeme kwa wananchi wa vijiji jirani kwa kuongeza nguzo 16 zilizobakia ili kuweza kupatikana kwa huduma hiyo kwa wananchi hao.




Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Tunguu Uwandani wakiwa katika eneo la hafla hiyo wakisikiliza nasaha zilizokuwa zikitolewa na wahusika.




Sheha wa Shehia ya Tunguu Uwangani akisoma dua baada ya hafla hiyo kumalizika ya kutowa shukrani




Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Maji Nishati na Mazingira Ally Halil Mirza Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu na Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar ZECO wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kijiji hicho baada ya kumalizika kwa hafla hiyo.




Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe, Simai Mohammed Said akizungumza na wananchi wa Jimbo lake baada ya kumalizika kwa hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad