Elimu : Tafiti ya HakiElimu yabaini Elimu Bure Imekuwa na Mafanikio Makubwa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


6 Apr 2017

Elimu : Tafiti ya HakiElimu yabaini Elimu Bure Imekuwa na Mafanikio Makubwa


Na Humphrey Shao,


Rais John Pombe Magufuli alipongia madarakani alitangaza elimu bure kwa shule za msingi na sekondari.


Taasisi ya Haki Elimu ni moja ya taasisi ambayo imefanya utafiti katika swala la elimu na kuja na majibu ambayo yameonesha kuwepo kwa mafanikio makubwa katika swala hili la elimu bure.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mapema leo,Mkurugenzi Mtendaji wa Haki Elimu, John Kalage ametaja kuwa tafiti hiyo imebaini kuwa Sera ya elimu bila malipo imesababisha ongezeko la wanafunzi wa darasa la kwanza hasa kwa shule za msingi.


“kulikuwa na ongezeko la asilimia 43 na asilimia 10 kwa shule za Sekondari ,hali iliyosababisha msongamano madarasani na pia kuongezeka kwa uwiano wa mwalimu kwa mwanafunzi kwa darasa la kwanza hadi kufikia mwalimu mmoja kufundisha wanafunzi 164 kwa wastani badala ya wanafunzi 45 wanaotakiwa” amesema Kalage.


Amesema kuwa utafiti huo ambao ulifanyika Wilaya za Njombe ,Mpwapwa , Sumbawanga ,Kilosa , Korogwe ,Tabora Mjini na Muleba kwa kuhusisha shule 28 na Msingi na 28 za Sekondari.


Amesema kuwa utafiti umebaini kuwa shule zenye wanafunzi wachache kati ya wanafunzi 200-300 zinapatiwa wastani wa Tsh 100,000-150,000 kwa mwezi ambayo hutatua matatizo ya msingi kama ukarabati hasa kuzingatia fedha za ruzuku zinatumwa shuleni kila mwezi.


Kalage amesema tafiti hiyo imetoa mapendekezo kwa serikali,ifanye jitihada za makusudi kuhakikisha kwamba wadau wote wanao elewa vizuri sera ya elimu bila malipo ili kurahisisha utekelezaji wake .


Amesema kuwa wadau wote wanapaswa kuzielewa nyaraka zote na miongozo kuhusiana na sera hii ili kila mdau atambue wajibu wake na jinsi anavyopaswa kushiriki katika utekelezaji wa elimu bure .


Amesema kutokana na elimu kuongeza kwa uandikishaji wa darasa la kwanza serikali ichukue hatua za makusudi kushughulikia changamoto zitakazotokana na elimu bila malipo kama vile ongezeko la wanafunzi , uhaba wa madarasa , walimu , Vitabu na Vinginevyo.


Ametaja kuwa zoezi la kupeleka fedha za ruzuku liende sambamba za serikali kutoa fedha za maendeleo kwa ajili yakuboresha miundombinu ya shule kwani shule nyingi zinachangamoto ya miundombinu na hivyo ni muda muafaka kwa serikali kuanza sasa kusaidia shule kwa kuzipa fedha za maendeleo kama amabvyo ilifanya wakati wa utekelezaji wa MMEM na MMES.

Mkurugenzi wa Haki Elimu nchini , John Kalage akizungumza na wadau mbalimbali wakati wa hafla ya uzinduzi wa tafiti juu ya mpango wa elimu bure nchini.

Aliyekuwa Mwenyekiti ya bodi ya taasisi ya Haki elimu nchini, Profesa Martha Qorro akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ripoti ya elimu bure iliyofanyiwa utafiti na tasisi ya Haki eleimu nchini

Baadhi ya washiriki wakisikiliza ripoti hiyo kwa makini

Dr. Richard Shukia kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam kitivo cha Elimu na Saikolojia akitoa maelezo juu ya tafiti hiyo

Wadau wakifatilia kwa makini maelezo kutoka kwa mtafiti

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad